Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Benki ya Exim Tanzania imewashauri wananchi kutumia huduma za fedha za kibenki kwa ajili ya usalama na maendeleo yao.
Wito huo ulitolewa jana na Meneja Uhusiano wa
Kibiashara wa Exim, Justin Wambali wakati wa ufunguzi wa mkutano wa siku
nne wa kibiashara na uwekezaji uliojumuisha wadau kutoka Israel na
Tanzania.
Mkutano huo uliambatana na Maonyesho ya Biashara
ya Tanzania- Israel Business and Investment Forum (TIBIF),
yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia mkutano wa TIBIF uliofunguliwa na
Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal alisema, umekutanisha wadau
kutoka taasisi za kibiashara na uwekezaji zinazojishughulisha na kilimo,
madini, huduma za fedha, elimu,miundombinu (barabara, maji), ujenzi na
makazi.
Mkutano huo umewakutanisha wadau zaidi ya 500
kutoka sekta za biashara, wawekezaji, watunga sera, viongozi katika
viwanda na watoa uamuzi kutoka kampuni mbalimbali na taasisi nyingine.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment