Home » » Miradi kukabili foleni yasuasua

Miradi kukabili foleni yasuasua

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mradi huu pia ungesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza msongamano kwani baadhi ya watu wangesafiri kwa kutumia kivuko au boti maalumu mpaka

Kasi ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kupunguza msongamano wa magari jijini Dar es Salaam inaonekana si ya kuridhisha licha ya ukubwa wa tatizo lenyewe.
Miradi hiyo ilitangazwa bungeni na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli katika hotuba yake ya Bajeti ya Mwaka 2013/2014.
Baadhi ya miradi iliyotangazwa na waziri ni pamoja na ujenzi wa barabara za juu kwenye makutano ya barabara  (flyover).
Mradi huu bado haujaanza kutekelezwa licha ya Dk. Magufuli kulieleza Bunge kuwa wakati ule walikuwa katika mchakato wa kumpata mkandarasi.
Mradi mwingine ni ujenzi wa kivuko au boti kutoka Dar es Salaam mpaka Bagamoyo chenye uwezo wa kubeba watu 300.
Mradi huu pia ungesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza msongamano kwani baadhi ya watu wangesafiri kwa kutumia kivuko au boti maalumu mpaka Bagamoyo.
Dk. Magufuli alisema katika hotuba yake kuwa mkandarasi wa mradi huo alikuwa amepatikana na usanifu wa maegesho matatu ulikuwa unaendelea.
Mpaka sasa hamna shughuli zozote zinazohusu mradi huo zinazoendelea, licha ya tamko hilo kutolewa na waziri mwenyewe.
Meneja wa Tanroads Mkoa wa Dar es Salaam, Julius Ndyamkama alisema ujenzi wa kivuko unaendelea mjini Bangladesh, India na mwezi wa tano kivuko hicho kitawasili nchini.
Ndyamkama alisema Tanroads wameanza maandalizi ya ujenzi wa Flyover maeneo ya Tazara na mpaka sasa wameondoa mabango ya matangazo, mabomba na nguzo za umeme  eneo ambako litajengwa daraja la juu.
“Kuhusu barabara alizozisema waziri, tayari makandarasi wameshapatikana na mikataba yote tuliyoingia ipo kwa Mwanasheria Mkuu. Utekelezaji utaanza baada ya Mwanasheria Mkuu kupitia mikataba hiyo,” alisema Ndyamkama.
Tatizo la msongamano wa magari Dar es Salaam  limeongezeka zaidi kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo  ujenzi wa mradi mwingine wa barabara za Mabasi Yaendayo Kasi (Dart).
Suluhisho la kudumu la  tatizo hili lingekuwa kufungua barabara nyingine ambazo pia zipo katika miradi ya wizara hiyo, ili kutoa nafasi ya kuendelea na ujenzi, wakati huohuo kupunguza foleni.
Ujenzi na upanuzi wa Barabara ya Morogoro (Mbezi) – Malamba Mawili – Kinyerezi – Banana bado unasuasua. Barabara hiyo ni mbaya, haijajengwa kwa kiwango cha lami.
Umuhimu wa barabara hii ni kupunguza msongamano wa magari katika Barabara za Mandela na Morogoro.
Barabara nyingine zilizo kwenye miradi ya wizara katika kupunguza msongamano Dar es Salaam ni ile ya kilomita 20 kutoka Tegeta–Kibaoni–Wazo– Goba – hadi Mbezi Mwisho.
Nyingine ni Kimara Baruti – Msewe - Changanyikeni, Tangi Bovu – Goba na Kimara – Kilungule – External (Mandela Road).
Katika barabara zote hizi, Dk. Magufuli alisema usanifu wake ulikuwa umekamilika.
Msemaji wa Wizara ya Ujenzi, Martin Ntemo alisema ujenzi wa barabara hizo ulichelewa kwa sababu mchakato wa kuwapata makandarasi unafanywa na wadhamini wenyewe ambao ni Wajapani.
Ntemo aliongeza kuwa ujenzi wa awamu ya pili wa barabara hizo utaanza muda wowote kwani makandarasi wameshapatikana.
“Tunatarajia kupokea kivuko kipya Mei mwaka huu. Kivuko hiki hakijachelewa, kimefuata taratibu zote kama ilivyotakiwa,” alisisitiza Ntemo.
Hata hivyo, kasi ya utekelezaji wa miradi hii haiendani  na ukubwa tatizo. Wengi wanatarajia kuwa barabara za mzunguko (ring roads) ambazo ni za muda mfupi zingejengwa haraka ili kusaidia wakati wa ujenzi wa miradi mikubwa ya muda mrefu.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa