Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA
YA MALIASILI NA UTALII
TAARIFA KWA UMMA
UZINDUZI WA SIKU YA TAIFA YA KUTUNDIKA MIZINGA
TAREHE 18 MACHI 2014
Siku ya Taifa ya Kutundika Mizinga itaadhimishwa
kitaifa mkoani Katavi katika wilayani Mlele tarehe 18 Machi 2014. Aidha, siku
hiyo mikoa mingine itaadhimisha kimkoa katika wilaya na vijiji
vilivyochaguliwa. Kauli Mbiu ya mwaka
huu ni: “Boresha Ufugaji Nyuki, Linda
Ubora wa Mazao Yake”.
Madhumini ya siku hii ni kuendeleza Ufugaji Nyuki
unaolenga kuongeza idadi ya wafuga nyuki, usimamizi bora wa makundi ya nyuki
na kuongeza uzalishaji wa mazao ya nyuki kwa kuzingatia ubora na teknolojia
za kisasa. Aidha, siku hii inatumika kuhamasisha uhifadhi endelevu wa
raslimali za misitu na nyuki.
Siku hii itakuwa chachu ya kuwahamasisha wadau na
wananchi kwa ujumla kushiriki kwa wingi katika ufugaji nyuki wa kisasa. Mgeni Rasmi atakuwa Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Kayanza
Peter Pinda (Mb), ambaye atashiriki kutundika mizinga katika msitu wa Mlele
Kusini eneo la Kanembela na baadaye kuhutubia wananchi.
Wizara ya Maliasili na Utalii inatoa wito kwa wadau na
wananchi kwa ujumla kushiriki kikamilifu katika kufanikisha siku hii kwenye
maeneo yaliyopangwa na maeneo binafsi.
MAENEO YATAKAYOTUNDIKWA MIZINGA KATIKA MIKOA MBALIMBALI
TANZANIA BARA
NA
|
MKOA
|
WILAYA
|
KIJIJI
|
MHUSIKA/
WAHUSIKA
|
ENEO
LA KUFUGIA
|
1
|
Simiyu
|
Busega
|
Mkula
|
Kikundi cha Imarika
|
Msitu wa Kikundi na Kijiji
|
2
|
Geita
|
Geita
|
Itina
|
Kikundi cha Itina
|
Msitu wa Kijiji (Ngitiri)
|
3
|
Mwanza
|
Ilemela
|
Kasamwa
|
Kikundi
|
Ngitiri ya kijiji
|
4
|
Mara
|
Musoma
|
|
Magereza
|
Msitu wa Magereza
|
5
|
Kagera
|
Missenyi
|
Kenyana
|
Kikundi cha Shubira
|
Miti katika Mashamba
|
6
|
Ruvuma
|
Songea
|
Mtyangimbole
|
Kamati ya Usimamizi Shirikishi
Misitu
|
Misitu wa Songea Fuel
|
7
|
Mtwara
|
Mtwara
|
Mnivata
|
Kikundia
|
Msitu wa Halmashauri
Mtiniko Mnivata
|
8
|
Lindi
|
Ruangwa
|
Liuguru
|
Kikundi cha Ufugaji Nyuki
|
Msitu wa Kijiji Liuguru
|
9
|
Iringa
|
Iringa
|
Mgera na Mngalali
|
|
Msitu wa Ubena
|
Mufundi
|
Shamba la Miti Sao Hill
|
Shamba la Miti Sao Hill
|
Shamba la Miti Sao Hill
|
10
|
Mbeya
|
Momba
|
Chilanu na Nzoka
|
Vikundi vya Ufugaji Nyuki
|
Mlima Malinde
|
11
|
Njombe
|
Ludewa
|
Mapogoro na Mavale
|
Vikundi vya Ufugaji nyuki
|
Msitu wa Sikaranyumbo
|
12
|
Rukwa
|
Kalambo
|
Kisumba, Kafukoka
|
Vikundi vya ufugaji nyuki
|
Msitu wa mto Kalambo
|
Nkasi
|
Vijiji (5) Chala A, B, na C,
Chalakima na Chatekelesha
|
Vikundi vya ufugaji nyuki kila
kijiji mizinga 10
|
Msitu wa Mlima Chale
|
13
|
Tanga
|
Korogwe
|
Mkwakwani Myusi
|
Kikundi cha Ufugaji Nyuki
|
Hifadhi ya asili Amani
|
14
|
Arusha
|
Arumeru
|
Nkwenankoli
|
Kamati ya Maliasili ya Kijiji
|
Hifadhi ya Msitu wa TFS
|
15
|
Kilimanjaro
|
Moshi
|
Kahe
|
NGO
|
Msitu wa Halmashauri
|
16
|
Tabora
|
Sikonge
|
Utyatya
|
Kikundi cha Wafugaji Nyuki
Nyahua
|
Bwawa la Utyatya
|
17
|
Kigoma
|
Uvinza
|
Uvinza
|
Kazaroho beekeepers
cooperative society
|
Msitu wa Basanza
|
18
|
Shinyanga
|
Shinyanga
|
Ukimbagu
|
NAFRAC na Kikundi cha Wafugaji
Nyuki Ugimbagu
|
Shamba la Albano Malila
|
19
|
Katavi
|
Mlele
|
Kanembela
|
Kikundi cha Ufugaji Nyuki
|
Msitu wa Mlele
|
20
|
Morogoro
|
Ulanga
|
Mselezi
|
Kikundi cha
ufugaji Nyuki SEMA
|
Msitu wa Hifadhi Mselezi
|
Gairo
|
Msingisi
|
TFS – Meneja Wilaya
|
Msitu wa Hifadhi Msingisi
|
21
|
Pwani
|
Bagamoyo
|
Msinune
|
Kikundi cha Ufugaji Nyuki
|
Msitu wa Simbo
|
Mkuranga
|
Kibuyuni
|
Kamati ya Maliasili na
Mazingira ya kijii
|
Msitu Masanganya
|
22
|
Dodoma
|
Kongwa
|
Nyamkonga
|
Kikundi cha Ufugaji Nyuki
|
Msitu wa Halmashauri ya Wilaya
|
23
|
Singida
|
Mkalama
|
Nkungi
|
Kikundi cha ufugaji Nyuki
|
Msitu wa Kijiji
|
24
|
Manyara
|
Babati
|
Haraa
|
Kikundi cha ufugaji Nyuki
|
Msitu wa Kijiji
|
|
Imetolewa na:
S.Gesimba
Naibu Katibu Mkuu,
Wizara ya
Maliasili na Utalii,
11/03/2014
0 comments:
Post a Comment