Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkurugenzi wa Sera,
Mpango na Utafiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt.
Raphael Kalinga akiwaeleza jambo waandishi wa Habari( Hawapo pichani) Wakati wa
Mkutano ulifanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari(MAELEZO) Leo Jijini Dar Es
Salaam.Kushoto ni Afisa Habari Mkuu wa Tume Hiyo Bi. Nadhifa Omar.
*********
Na Hassan Silayo-MAELEZO
Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS)
imedhamiria kuanzisha Mfuko wa Ukimwi utakaolenga kuondoa upungufu wa
Rasilimali katika maeneo mbalimbali ili kuboresha afua za ukimwi nchini.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Sera, Mpango na
Utafiti wa Tume hiyo Dkt. Raphael Kalinga leo Jijini Dar es Salaam.
Dkt. Kalinga alisema kuwa uanzishwaji wa Mfuko huo
ni moja yakipaumbele kilichowekwa na Tume hiyo katika kuimarisha uratibu wa
utekelezaji wa mkakati wa taifa wa kudhibiti Ukimwi kwa mwaka wa Fedha 2014/2015.
“Katika kuendelea kuimarisha uratibu wa utekelezaji
wa mkakati wa taifa wa kudhibiti Ukimwi
kwa mwaka wa Fedha 2014/2015 Tume imeamua kuweka vipaumbele ikiwamo
kuanzisha mfuko wa UKIMWI( ATF) utakaolenga kuondoa upungufu wa Rasilimali
katika maeneo mbalimbali ili kuboresha afua za ukimwi nchini” Alisema Dkt.
Kalinga.
Aidha Dkt. Kalinga aliongeza kuwa mfuko huo
unategemewa kuaza ifikapo Julai, 2015 na kuanza jukumu la kuhamasisha utafutaji
wa Rasilimali za kudhibiti Ukimwi Nchini.
Pia Dkt. Kalinga alibainisha kuwa Tume itaendelea
kutoa kipaumbele cha afua za Vijana hasa walio katika umri kati ya miaka 15
hadi 24 waliopo shuleni na nje ya shule kwa kuwa ndio kundi lenye changamoto ya
rika balehe na pia ufahamu mdogo ambao ni sawa na asilimia 40.3 kwa wanawake na
47.3 kwa wanaume kwenye masuala ya ukimwi.
Pia Dkt. Kalinga aliongeza kuwa kundi hilo halina
hamasa hasa katika masuala ya upimaji wa Ukimwi na Matumizi ya kinga, baadhi
wanajihusisha na tabia hatarishi ikiwamo kujiunga na makundi hatarishi,
wanachangia kwa asilimia kubwa maambukizi ya ukimwi kulingana na utafiti wa
viashiria vya ukimwi na malaria wa Mwaka 2011/2012.
TACAIDS imepanga kuhamasisha Halmashauri zote nchini
kutenga fedha za udhibiti UKIMWI kutoka kwenye vyanzo vya mapato ya Ndani.
0 comments:
Post a Comment