Home » » 13 MBARONI WAKITUHUMIWA KUIBA MABILIONI BARCLAYS

13 MBARONI WAKITUHUMIWA KUIBA MABILIONI BARCLAYS

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 13 wanaodaiwa kuhusika katika tukio la ujambazi uliofanyika katika Benki ya Barclays Tawi la Kinondoni hivi karibuni ambapo kiasi cha sh. 390,220,000, dola 55,000, euro 2,150 na vitabu vya hudi 50 viliibwa.
Miongoni mwa wanaoshikiliwa na jeshi hilo ni wanawake wawili ambao ni mameneja wa Barclays, tawi la Kinondoni ulipofanyika wizi huo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, aliwataka mameneja wa tawi hilo wanaoshikiliwa Alune Kasililika (28) na mwenzake ambaye ni Meneja Uendeshaji, Neema Bandari.
Watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa ni Frederick Lazaro (19), Kakamiye Julius (31), Idd Nguvu (32)Sazery Osward, Boniface Ndaro (29)na Erasimus Berbard (38).
Kamanda Kova aliwataja wengine kuwa ni Deo Isdory (32), Mohamed Athuman (31) Licy Amos (30) na Grace Amon (39).Alisema tukio hilo lilifanyika Aprili 15 mwaka huu saa tatu na nusu asubuhi katika tawi la Kinondoni.
Alisema siku ya tukio watu waliokuwa na silaha aina ya SMG na Bastola waliingia ndani ya benki na kupora kiasi hicho cha fedha.
Kamanda Kova, alisema baada ya kutokea wizi huo Jeshi la Polisi liliuda kikosi maalum cha upelelezi (Task Force) na kugundua kwamba robo tatu ya fedha zote zilizoibwa zilichukuliwa kabla ya siku ya tukio la ujambazi huo.
Alisema kuwa majambazi hao walifika eneo la tukio na kuwatishia kwa silaha watumishi wa benki hiyo na kuwaweka chini ya ulinzi na hatimaye kutoroka na pesa hizo kwa kutumia pikipiki aina ya Fekon.
Kamanda alisema kuwa Jeshi la Polisi limegundua kuwa wizi huo unaohusisha mabenki umekuwa ukihusisha wafanyakazi wenyewe pamoja na mameneja wao

Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa