Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Drive Dantsu, Cheriff Tabet (wa tatu kulia), akiwa na viongozi mbalimba wa kampuni hiyo wakati wa kutambulisha kwa wanahabari kufunguliwa kwa ofisi hiyo nchini Dar es Salaam jana.(Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
Dotto Mwaibale
KAMPUNI ya Drive Dentsu imepiga hodi kwa kufungua
ofisi zake jijini Dar es Salaam ikiwa ni jitihada za kusogeza huduma zake kwa wateja wake
katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari
Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Cherrif Tabet alisema
kampuni hiyo iliyotanda nchi takriban 110 ni sehemu ya muunganiko wa kimataifa
wenye zaidi ya wafanyakazi 37000 na ofisi 160 duniani kote.
"Ni muungano ambao unaleta pamoja ujuzi, maarifa na vitendea kazi vyenye kuhakikisha inawapa wateja wake huduma zenye ubora wa hali ya juu" alisema Tabet.
Alisema ufunguzi wa ofisi hiyo jijini Dar es
Salaam umelenga kutoa suluhisho la ubunifu kwa makampuni na bidhaa za
kitanzania.
Tabet alisema pamoja na kuwekeza hapa nchini
kampuni hiyo imelenga kujipanua katika masoko mengine katika ukanda wa Afrika
Mashariki ili kuhakikisha wanakidhi mahaitajai yao kwa kutoa sukluhu kwa
changamoto zote za kibiashara.
"Katika ukanda wa Afrika Mashariki, uchumi
wa Tanzania umekuwa ukikua kwa kasi kubwa pamoja na ongezeko la uzarishaji wa
bidhaa nyingi jambo ambalo linakuza mazingira yenye ushindani hivyo kufanya
kuwepo na uhitaji mkubwa wa ubunifu katika kuwafikia wateja" alisema
Tabet.
Meneja Mkuu wa Masoko na Maendeleo ya Biashara wa
kampuni hiyo, Rami El Khalil alaisema Tanzania ni nchi yenye fursa nyingi
kutokana na uchumi wake kuwa imara hivyo ni sehemu nzuri kuwekeza.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment