Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » MAONYESHO YA BIDHAA ZA KICHINA KUFANYIKA DAR

MAONYESHO YA BIDHAA ZA KICHINA KUFANYIKA DAR

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 

MAONYESHO ya bidhaa za Kichina yanatarajiwa kufanyika Agosti 21 hadi 24 mwaka huu kwa madhumuni ya kuendeleza uhusiano uliopo kati ya Tanzania na China hususani katika masuala ya biashara.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jana,mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya viwanda, biashara na Kilimo, Bw.Daniel Machembe alisema kuwa maonyesho hayo yanatarajia kufanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam.

Alisema kuwa maonyesho hayo ni kwa ajili ya kuendeleza uhusiano uliopo kati ya Tanzania na China hususani katika masuala ya biashara ambapo sasa yanafanyika kwa mara ya tatu katika mwaka huu.

Alisema kuwa maonyesho ya mwaka huu yanatarajia kuhusisha bidhaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na mashine,magari, vifaa vya nyumbani,vifaa vya umeme pamoja na vifaa vya ujenzi.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa kumekuwa na uhusiano mzuri baina ya Tanzania na China tangu mwaka 2001 ambapo Tanzania ilianza kupeleka bidhaa mbalimbali kuuza nchini humo kwa ajili ya kuingizia pato Taifa.

Alisema kuwa Watanzania wanatakiwa kuwa na utamaduni wa kupenda bidhaa zenye ubora.

Alisema kuwa China imepata fursa nzuri kwa ajili ya kufanya maonyesho ya bidhaa zao Tanzania kwa ajili ya kuendeleza na kukuza uchumi.

Alisema kuwa thamani ya biashara kati ya China na Tanzania mwaka jana ilifikia dola za Kimarekani bilioni 3.7 ambayo imezidi kwa asilimia 49 kuliko ilivyokuwa mwaka 2012 na kuweka rekodi mpya.

"Tunatarajia bidhaa za mwaka huu zitaendelea kuwa bora kutokana na urafiki wa muda mrefu uliopo kati ya China na Tanzania, kwani China imekuwa ikifanya maonyesho nchini kwa ajili ya kukutana na Wafanyabiashara wakubwa na kuwauzia bidhaa mbalimbali," alisema.

Chanzo;Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa