Home » » 'PANYA ROAD' 1,289 WATIWA MBARONI DAR

'PANYA ROAD' 1,289 WATIWA MBARONI DAR

Suleiman Kova, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam
.
Idadi ya vijana wanajihusisha na kundi la uhalifu maarufu kama ‘panya road’ imeongezeka na kufikia 1,289 kwa mikoa yote mitatu mkoani Dar  es  Salaam.
Kati yao vijana 163 toka katika manispaa za Temeke na Kinondoni wamefanyiwa uchunguzi, na muda wowote kuanzia sasa wanatarajiwa kufikishwa mahakamani.

Vijana hao waliokamatwa ni pamoja na wapiga debe katika vituo vya daladala, wacheza kamari, wavuta bangi, watumiaji wa dawa za kulevya na watumiaji wa pombe haramu ya gongo.

Akizungumza na NIPASHE jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, alisema tangu Januari  5 hadi 7, mwaka huu wamekamatwa Panya road 240 na kati yao, 95 uchunguzi wao umekamilika na watafikishwa mahakamani muda wowote kuanzia sasa.

“Operesheni hii ni endelevu, lengo ni kufuta kabisa jina la  Panya road pamoja na kuondoa makundi yote ya wazururaji, wavuta bangi, dawa za kulevya pamoja na watumiaji wa pombe haramu ya gongo,” alisema.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Kihenya Kihenya, alisema juzi  waliwakamata vijana 57 ambapo ma kufikisha jumla ya waliokamatwa 225 na kati yao 68 uchunguzi dhidi yao umekamilika na watapelekwa mahakami muda wowote.

Baada ya kundi hilo kutikisa  Jiji la Dar es Salaam,Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya  Dar es Salaam lilianzisha kamatakamata na  operesheni Jiji zima kwa lengo   la kukabiliana na makundi hayo ya kihalifu hasa kundi hilo.
 
CHANZO: NIPASHE
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa