Home » » Wajumbe kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali wakutana kujadili maazimio yaliyofikiwa kuhusu suala la Bei za Filamu.

Wajumbe kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali wakutana kujadili maazimio yaliyofikiwa kuhusu suala la Bei za Filamu.


Wajumbe kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali jana walikutana katika ofisi za Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo kuzungumzia maazimio yaliyofikiwa kutoka katika kikao cha kwanza kilichowakutanisha wasambazaji wa filamu wakiwasilisha malalamiko yao kwa mheshimiwa waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo.

Wajumbe hao kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Wizara ya Viwanda na Biashara,Wizara ya fedha,Shirika la Mapato Tanzania(TRA),Shirika la Viwango Tanzania(TBS) na  Tume ya Ushindani walizungumzia kwa mapana maazimio hayo kumi tatu(13) kama kutoa ushauri kwa kampuni mbalimbali za simu kuchangia maendeleo ya wasanii wanaowatumia,Shirika la Mapato Tanzania pia liongeze udhibiti katika filamu za nje zinazoingizwa nchini na filamu hizo zifuate sheria,kanuni na Taratibu kabla ya kuingizwa sokoni na kukazia swala la hakimiliki iongezwe nguvu ili iweze kupambana na suala la uharamia.

Akitoa hoja katika majadiliano hayo Katibu mtendaji  wa Bodi ya filamu Bi.Joyce Fissoo alishauri Shirika la Mapato Tanzania kuendelea kutoza kodi filamu za nje kwani zitalinda viwango vya filamu izi na pia udhibiti uongezeke katika uingizaji wa filamu za nje.

Nae Afisa Mtendaji Mkuu  kutoka COSOTA  Bi. Doreen Sinare aliwasihi wasanii kuwa makini na kuuza hakimiliki za kazi zao na kukazia kwamba chama cha hakimiliki kipo kwa ajili yao kwaiyo wasisite kuwatembelea kwa ajili ya ushauri wa kisheria na pia kusajiri kazi zao cosota.

Kwa upande wake mjumbe kutoka Tume ya ushindani Bi.Martha Kisombe alisisitiza kuwa  chombo chao kipo kwa ajili ya kulinda na kukuza ushindani katika soko na kumlinda mlaji kutokana na masuala yote yasiyo na usawa na upotoshaji wa kimauzo.

Aidha ,Afisa Viwango kutoka Shirika la Viwango nchini Bw.Henry Massawe alieleza upande wao wataendelea kusimamia viwango katika soko la Filamu ili kupata kitu bora pamoja na kusimamia CD/DVD zinazotoka nje ziwe na kiwango kizuri.

Kikao hicho cha wajumbe kilikutana pia na wasambazaji wa filamu ili kuwapa mrejesho wa maazimio waliyofikia katika kikao cha kwanza  ambapo kikao hicho kilihairishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya maendeleo ya Utamaduni Bi.Lilly Beleku kutokana na wasambazaji hao kuja na zaidi ya watu walioalikwa katika kikao hicho na hata alipowaomba kutoka wale wasiohusika walipinga.

Hivi karibuni baadhi ya  wasambazaji wa Filamu waliwasilisha pendekezo lao kwa Serikali kufuatia kampuni ya  Steps  entertainment  kutangaza kutaka kushusha bei ya mauzo ya filamu mpaka  shilingi 1000,wazo ambalo baadhi ya wasambazaji  na wasanii wamelipinga
 Katibu Bodi ya Filamu Tanzania Bi,Joyce Fissoo(kushoto) akiskiliza hoja mbalimbali kutoka kwa wajumbe(hawapo pichani) wa kikao kilichofanyika leo kuhusu suala zima la bei za filamu,kulia ni Kaimu mkurugenzi wa idara ya Maendeleo ya  Utamaduni Bi.Lilly Beleku.

 :Wajumbe kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Fedha wakiwa katika kikao cha Pamoja wakijadili suala zima la bei za Filamu leo jijini Dar es Salaam ambapo baadhi ya  wasambazaji na wasanii wa filamu walilalamikia maamuzi ya kutaka kushushwa kwa bei kutoka kampuni ya Steps Entertainment kwamba hauna Tija na ivyo kulileta swala ilo kwa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo.
 Baadhi ya wajumbe waliohudhuria kikao ili kujadili suala la bei za filamu wakiwa wanamskiliza Kaimu mkurugenzi wa Utamaduni(hayupo pichani),Bi.Lilly Beleku walipokuwa wakijadili swala zima la bei za filamu wakizungumzia haswa kuzingatiwa kwa bei kutokuwa chini sana kuliko gharama za uzalishaji.
 Afisa Mtendaji Mkuu kutoka COSOTA,Bi Doreen Sinare akielezea jinsi wanavyowasaidia wasanii kwa kuwapa ushauri unaofaa katika kazi zao na swala zima la uharamia katika tasnia nzima ya filamu.
 Wajumbe kutoka bodi ya filamu wakimskiliza kwa makini Dkt. Mona Mwakalinga(aliyevaa Miwani) kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam Idara ya sanaa na maigizo walipokuwa wakizungumzia swala zima la ukuaji wa filamu nchini na Bei zake kwa ujumla.

 Wajumbe waliohudhuria kikao cha majadiliano ya maadhimio yanayohusu bei za filamu wakiskiliza kwa makini maadhimio yaliyofikiwa katika kikao cha kwanza.


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa