Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » MWILI WA MKE WA MWANAHABARI THOBIAS MWANAKATWE WA KAMPUNI YA THE GUARDIAN ALIYEFARIKI KWA KUGONGWA NA GARI NJE YA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA JULIUS NYERERE WAAGWA JIJINI DAR ES SALAAM KUZIKWA KARATU MKOANI ARUSHA

MWILI WA MKE WA MWANAHABARI THOBIAS MWANAKATWE WA KAMPUNI YA THE GUARDIAN ALIYEFARIKI KWA KUGONGWA NA GARI NJE YA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA JULIUS NYERERE WAAGWA JIJINI DAR ES SALAAM KUZIKWA KARATU MKOANI ARUSHA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Mhariri wa Gazeti la Nipashe, Jesse Kwayu (kushoto), na waombolezaji wengine wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa mke wa mwanahabari wa Kampuni ya The Guardian, Thobias Mwanakatwe, Levina Genda wakati wakilipekeka kwenye gari tayari kwa safari ya kwenda Karatu mkoani Arusha kwa mazishi yatakayofanyika kesho.
 Mwanahabari wa Kampuni ya The Guardin Ltd, Thobias Mwanakatwe akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa mke wake, Levina Genda wakati wa ibada ya kumuaga iliyofanyika Hospatali ya Amana Dar es Salaam leo a. Mke wa Mwanakatwe alifariki kwa kugongwa na gari maeneo ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mwishoni mwa wiki.
 Waombolezaji wakiwa kwenye ibada ya kumuaga Levina Genda, iliyofanyika Hospitali ya Amana Ilala Dar es Salaam leo asubuhi.
 Hapa ni huzuni umetawala.
 Wafanyakazi wenzake na Thobias Mwanakatwe wa Kampuni ya The Guardian wakiwa wamejiinamia kwa huzuni.
 Thobias Mwanakatwe (katikati), akiwa na wafanyakazi wenzake waliofika kumfariji.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Levina na waombolezaji wengine wakiwa kwenye ibada ya kumuaga mpendwa wao.
 Kiongozi wa dini kutoka kanisa la Katoliki akiongoza ibada ya kumuombea marehemu.
 Ibada ikiendelea.
 Mwakilishi wa wanahabari kutoka mkoani Mbeya ambako Mwanakatwe alikuwa akifanyakazi kabla ya kuhamia Dar es Salaam, Patrick Kosima akitoa akizungumza katika ibada hiyo kabla ya kutoa rambirambi ya sh.220,000.
 Mhariri wa Gazeti la Nipashe, Jesse Kwayu (katikati), akizungumza katika ibada hiyo wakati akiwasilisha salamu za rambirambi za Kampuni ya The Guardian.
 Mdau Fabiola Bula wa Karatu, akitoa heshima za mwisho kwa marehemu. 
 Heshima za mwisho kwa marehemu zikiendelea.
 Wafanyakazi wa Kampuni ya The Guardian wakitoa heshima za mwisho kwa wifi yao, Levina Genda. 'Hakika ni huzuni tupu'
Jeneza likiingizwa kwenye gari tayari kwa safari ya kwenda Karatu kwa mazishi.
(Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com-simu namba -0712-727062)

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa