Na
Nyakongo Manyama-Maelezo
Tarehe
: 30/11/2015.
Dar
es Salaam.
Kufuatia
agizo laWaziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa la kuwataka watuhumiwa wa wizi wa
makontena 329 katika bandari ya Dar es salaam kuchukuliwa hatua na Jeshi la Polisi,
tayari Jeshi hilo limewashikilia watuhumiwa kumi na mbili wanaohusika na wizi
huo.
Akiongea
na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (CP)
Diwani Athumani amesema kuwa, uchunguzi unaofanywa na wataalamu waliobobea katika
makosa ya uhalifu wa kifedha umeweza kuwabaini watu kumi na mbili ambao wamehusika na wizi huo.
“Kati
ya watuhumiwa hao kumi na mbili, watano wanashikiliwa na Jeshi la Polisi na
saba bado wapo katika upepelezi na upelelezi utakapokamilika watafikishwa
mahakamani,” alisema Kamanda Athumani.
Wanaoshikiliwa
kutokana na tuhuma mbalimbali ni Kamishna wa Idara ya Forodha na Ushuru TRA Bw.
Tiagi Masamaki, Meneja Kitengo cha Huduma za Ushuru na Bi. Habib
Mponezia, Msimamizi Mkuu wa Kitengo cha Ushuru wa Forodha.
Watuhumiwa
wengine ni pamoja na Bi. Eliaichi Mrema, Msimamizi Kitengo cha Mawasiliano ya Kompyuta
Bw. Haroun Mpande na Mchambuzi Mwandamizi wa Masuala ya Biashara
Bw. Hamis Omary.
Aidha
Kamanda Athumani amewaomba wananchi wenye taarifa za ubadhilifu wa mali za Umma
kuendelea kulisaidia Jeshi la Polisi katika kutekeleza majukumu yake.
0 comments:
Post a Comment