Na
Shamimu Nyaki-Maelezo
Jeshi
la polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam limewakamata wahamiaji haramu 105 raia
wa Ethiopia kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria wakiwa wanasafirishwa
kwenda nchi nyingine za Afrika.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Kamanda wa Polisi kanda maalumu ya Dar es
Salaamu Kamishna Suleiman Kova amesema wahamiaji hao ambao wote ni wanaume
wamekamatwa kutokana na ushirikiano wa wasamaria wema wanaoshi eneo hilo la
Tabata Segerea.
Ameongeza
kuwa wahamiaji hao waliingia nchini ya usimamizi wa mwanamke mmoja anaeitwa
Zainabu Umwiza (25) anaesemekana ni raia wa nchi ya Burundi ambae anajihusisha
na biashara hiyo ya usafirishaji haramu wa binadamu ambao ni kosa la jinai
tayari kuwapeleka nchi nyingine na hivyo amemuomba ajisalimishe
“ Bi
Zainabu Umwiza mwenye asili ya Burundi tunamwomba ajisalimishe maana yeye ni
mfanyabiashara wa usafirishaji wa binaadamu
kutoka nchi za Afrika kwenda Ulaya” kamanda Kova alisisitiza.
Aidha
kamanda Kova ameeleza kuwa polisi walifanya upekuzi katika nyumba ya mwanamke
huyo ndipo walipowakuta wahamiaji hao ambapo uchunguzi wa awali unaonyesha
kwamba, usafirishaji wa binadamu kutoka Afrika kwenda bara la Ulaya unaofanywa
na mwanamke huyo, ambao hufanyika kwa malipo ya Dolla 1000 kwa mtu mmoja.
Kamanda
Kova ameongeza kuwa watuhumiwa hao walipohojiwa kujua kwamba wana kibali
chochote cha kuingia nchini waligunduliwa kuwa hawana na kueleza kuwa waliingia
kupitia njia za panya na mbinu nyingine ambazo bado zinachunguzwa na kwamba
wamewajulisha idara ya Uhamiaji na
watashirikiana nao katika upelelezi ili hatimaye sheria ichukue mkondo wake.
Hata
hivyo amewataka wananchi kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi katika
kundoa na kuzuia tatizo la wahamiaji haramu ambao wamekua tishio katika usalama
wa maisha ya wananchi na mali zao.
0 comments:
Post a Comment