Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Saidi Meck Sadik amesema kwamba sera ya
elimu bure imewezesha wazazi kote nchini kuweza kuandikisha watoto
shule jambo ambalo limepandisha idadi ya uandikishaji wa darasa la
kwanza mara dufu.
Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo alipokuwa akizungumza katika mkutano
ulioandaliwa na wazee wa jiji la Dar es salaam kwa ajili ya kumpongeza
Rais Dkt. Magufuli kwa kukaa madarakani kwa siku 100 huku akitekeleza
ilani ya Chama cha Mapinduzi.
Ameongeza kuwa katika shule ya msingi Maji matitu jijini Dar es
salaam imeweza kuandikisha wanafunzi 1,022 wa darasa la kwanza na
kuvunja rekodi ya shule zote hapa nchini, Pia shule hiyo moja ina
wanafunzi 5823 jambo ambalo kwa mujibu wa viwango vya elimu kwa idadi
hiyo ya wanafunzi hao wanatosha kuanzisha shule 6.
Kwa kutambua upungufu uliopo katika shule hiyo kuanzia siku ya
jumatatu serikali kupitia mkoa wa Dar es salaam itajenga madarasa 10
katika shule ya Majimatitu wilayani Temeke.Pia Mkoa utajenga madarasa
500 katika manispaa za Ilala,Kinondoni na Temeke ili kuhimili kishindo
cha wanafunzi walioandikishwa.
Aisha Mkuu wa mkoa amewataka watanzania wote kumuunga mkono Rais
Magufuli katika utumishi wake na kuepuka kumkatisha tamaa kwani nchi
inayojengwa ni moja hakuna haja ya kugombea fito.
0 comments:
Post a Comment