Frank Mvungi
- MAELEZO
TAKUKURU
yawahamasisha wananchi kushishiriki
kampeni ya LONGA NASI ili kukomesha
vitendo vya rushwa hapa nchini.
Kauli hiyo
imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkuu wa Sehemu ya Uratibu na utoaji
Habari,Idara ya Elimu kwa Umma toka Taasisi ya Kuzuia na Kupmbana na rushwa
(TAKUKURU) Bw. Matai Kirumbi wakati wa mkutano na vyombo vya Habari.
Akizungumzia
Kampeni hiyo, Kirumbi amesema inalenga
kuwajengea uelewa wananchi kuhusu mapambano dhidi ya rushwa ili kuzuia vitendo
vya rushwa .
Katika
Kampeni hiyo wananchi wanatakiwa kutoa taarifa za kuwepo kwa vitendo vya rushwa
au viashiria vyake kwa kupiga namba 113 au *113# kupitia simu ya kiganjani .
Huduma hiyo inapatikana kupitia mitandao ya AIRTEL,TIGO,HALOTEL,VODACOM
na ZANTEL ambapo wananchi hawatatozwa
gharama yoyote.
“Taarifa
8000 zimeshapokelewa na Taasisi yetu tangu kuzinduliwa kwa Kampeni hii na
nyingi ni za wananchi kuombwa hongo na tayari tunazifanyia kazi “alisisitiza
Kirumbi.
Akifafanua
kuhusu taarifa hizo Kirumbi amesema kuwa zinaonyesha wananchi wamepokea vizuri
kamapeni hiyo iliyozinduliwa tarehe 24/5/2016 na Makamu wa Rais Mh. Samia
Suluhu Hassan.
Katika
kampeni hiyo wananchi watajengewa ujasiri zaidi ili kuongeza ushiriki wao
katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kutoa taarifa na kutoa mrejesho wa kero
zilizotatuliwa.
Matarajio ni
kuongezeka kwa ubora wa huduma za jamii kwa kuwa fedha za umma zitatumika kama
ilivyopangwa katika huduma kama vile kununua dawa.
Akizindua
kampeni ya LONGA NASI jumanne tarehe 24,Mei 2016 katika viwanja vya Mwembeyanga
Wilayani Temeke Jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan
alisisitiza suala la ushiriki wa kila mmoja katika mapambano dhidi ya rushwa
nchini alisema”Tunahitaji nguvu za
pamoja ili kumaliza tatizo la rushwa nchini”.
………Mwisho…….
0 comments:
Post a Comment