Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » TAKUKURU yawahamasisha wananchi kushishiriki kampeni ya LONGA NASI

TAKUKURU yawahamasisha wananchi kushishiriki kampeni ya LONGA NASI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 




Frank Mvungi - MAELEZO
TAKUKURU yawahamasisha wananchi  kushishiriki kampeni ya LONGA NASI  ili kukomesha vitendo vya rushwa hapa nchini.
Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkuu wa Sehemu ya Uratibu na utoaji Habari,Idara ya Elimu kwa Umma toka Taasisi ya Kuzuia na Kupmbana na rushwa (TAKUKURU) Bw. Matai Kirumbi wakati wa mkutano na vyombo vya Habari.
Akizungumzia Kampeni hiyo,  Kirumbi amesema inalenga kuwajengea uelewa wananchi kuhusu mapambano dhidi ya rushwa ili kuzuia vitendo vya rushwa .
Katika Kampeni hiyo wananchi wanatakiwa kutoa taarifa za kuwepo kwa vitendo vya rushwa au viashiria vyake kwa kupiga namba 113 au *113# kupitia simu  ya kiganjani .
Huduma hiyo  inapatikana kupitia mitandao ya AIRTEL,TIGO,HALOTEL,VODACOM na  ZANTEL ambapo wananchi hawatatozwa gharama yoyote.
“Taarifa 8000 zimeshapokelewa na Taasisi yetu tangu kuzinduliwa kwa Kampeni hii na nyingi ni za wananchi kuombwa hongo na tayari tunazifanyia kazi “alisisitiza Kirumbi.
Akifafanua kuhusu taarifa hizo Kirumbi amesema kuwa zinaonyesha wananchi wamepokea vizuri kamapeni hiyo iliyozinduliwa tarehe 24/5/2016 na Makamu wa Rais Mh. Samia Suluhu Hassan.
Katika kampeni hiyo wananchi watajengewa ujasiri zaidi ili kuongeza ushiriki wao katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kutoa taarifa na kutoa mrejesho wa kero zilizotatuliwa.
Matarajio ni kuongezeka kwa ubora wa huduma za jamii kwa kuwa fedha za umma zitatumika kama ilivyopangwa katika huduma kama vile kununua dawa.
Akizindua kampeni ya LONGA NASI jumanne tarehe 24,Mei 2016 katika viwanja vya Mwembeyanga Wilayani Temeke Jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan alisisitiza suala la ushiriki wa kila mmoja katika mapambano dhidi ya rushwa nchini alisema”Tunahitaji nguvu za pamoja ili kumaliza tatizo la rushwa nchini”.
 ………Mwisho…….

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa