SERIKALI YASAINI HATI YA MAKUBALIANO YA BILIONI
440 NA BENKI YA DUNIA
Na
Benny Mwaipaja, WFM
Serikali
kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imesaini hati ya makubaliano na Benki ya
Dunia itayoiwezesha Tanzania kupata nyongeza ya fedha katika mradi wa Tasaf kiasi
cha Shilingi Bilioni 440.
Hati
hiyo ilisainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius
Likwelile na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Bella Bird, Makao Makuu ya
Wizara ya Fedha, Dar es Salaam, leo, Juni 23, 2016.
Akiongea
wakati wa kusaini hati hiyo Dkt. Likwelile alisema kuwa fedha hizo zitaelekezwa
katika mradi wa Tasaf II kwa ajili ya kuziwezesha kaya maskini kukuza kipato
chao kupitia ajira za muda zitakazowawezesha kupeleka watoto shule na kuwapatia
huduma za afya.
Aliongeza
kuwa katika mwaka wa fedha 2015/2016 Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia
imefanya kazi kubwa iliyowezesha miradi kumi kupitishwa ambayo ina thamani ya
Shilingi Trilioni 1.9.
"Miongoni
mwa miradi iliyopata ufadhili ni pamoja na mradi wa kuboresha mazingira ya
biashara uliopata shilingi Bilioni 168, mradi wa kusambaza umeme vijijini (REA),
uliopata Shilingi Bilioni 440" Aliongeza Dkt. Likwelile
Aidha,
alisema kuwa Serikali inaendelea na majadiliano na Benki hiyo kwa ajili ya
kuboresha Bandari ya Dar es Salaam, ambapo kiasi cha dola Milioni 600
zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.
Dkt.
Likwelile ameishukuru Benki ya Dunia kwa mchango wake mkubwa na kusema kuwa
Serikali itahakikisha kuwa inazisimamia taasisi zinazotekeleza miradi hiyo ili
ziweze kutumia fedha hizo vizuri na kwa malengo yaliyokusudiwa.
Kwa
upande wake Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bella Bird, amepongeza juhudi
za Serikali ya awamu ya tano katika kupambana na rushwa na kuweka mazingira rafiki kwa sekta binafsi.
Aliongeza
kuwa sekta binafsi ndizo zinatoa ajira kwa wingi na kusaidia kuchangia katika
kuongeza mapato ya Serikali.
Ameahidi
kuwa Benki yake itaendelea kushirikiana na Tanzania ili kuiwezesha kufikia
malengo yake ya kiuchumi na kijamii kwa faida ya wananchi wake.
0 comments:
Post a Comment