Shirika lisilo la kiserikali, International Organization for Migration,(IOM) limeendesha
mafunzo ya siku moja kwa zaidi ya vijana 150 waliyopo katika Vyuo Vikuu,Sekondari
na wale wa mitaani lengo ni kuwapa elimu
na kufahamu faida za kiusalama za
Uhamaji.
Akifungua mafunzo hayo katika, Hotel Coral Beach iliyopo
Masaki jijini ,Afisa Miradi wa shirika hilo Charles Mkude, amesema kuwa lengo
la kuwakutanisha vijana hao ili kuwajengea uwezo wa kutambua mambo mbalimbali
yatokana na Uhamaji na kujua faida na hasara zake.
“Uhamaji sio tatizo la nchi pekee, bali tatizo la ulimwengu
mzima ni wajibu wetu kufanya hivi kila mara maana kundi kubwa la vijana
wakielimishwa basi kama taifa tunaweza kupiga hatua moja mbele lengo kubwa ni
kueleza maswala jinsi gani jamii inaweza kufaidika na uhamaji kwa fuata taratibu sahihi za kiusalama,unajua wengi utumia mwaya
huu uhamaji kwa kufanya biashara haramu za utumwa katika mataifa mbalimbali iwapo kila
kijana ataelewa kwa kina kuhusu mafunzo haya basi atapeleka ujumbe katika
jamiii na kuwa barozi mzuri ili mwisho wa siku yatumike maamuzi ya kibusara
kama taifa”alisema Mkude.
0 comments:
Post a Comment