Home » » “Serikali haitamvumilia mtumishi wa afya anayefanya kazi bila kuzingatia weledi na maadili ya kazi yake”

“Serikali haitamvumilia mtumishi wa afya anayefanya kazi bila kuzingatia weledi na maadili ya kazi yake”

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

AF1 
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi, akizungumza na waandishi wa habari nje ya Ukumbi unaofanyika Mkutano wa Pili wa Neuroradiolojia  jijini Dar es Salaam, unaojadili Jukumu la Neuroradiolojia katika kukapambana na Magonjwa Yasiyoambukiza.
AF2 
Msajili Mstaafu wa Baraza la Wataalamu wa Radiolojia (MRIPC) Euniace Bandio, akizungumza kuwakaribisha Wataalamu na Washiriki wa Mkutano wa Pili wa Neuroradiolojia unaofanyika jijini Dar es Salaam. Mkutano huo wa siku mbili unajadili Jukumu la Neuroradiolojia katika kukapambana na Magonjwa Yasiyoambukiza.
AF3 
Katibu wa Jukwaa la Neuro-rad Dkt. Mboka Jacob akizungumza na washiriki wa mkutano wa Pili wa Neuroradiolojia  unaofanyika jijini Dar es Salaam.
AF4 
Baadhi ya watalaamu wa Radiolojia na washiriiki wa mkutano huo wakimsikiliza mgeni rasmi.


Hussein Makame-MAELEZO
SERIKALI imesema haitamvumilia mtumishi yeyote wa sekta ya afya atakayefanya kazi zake bila kuzingatia weledi na maadili ya taaluma za sekta hiyo.
Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi, wakati akifungua Mkutano wa Pili wa Neuroradiolojia  ulioanza jijini Dar es Salaam leo, kujadli Jukumu la Neuroradiolojia katika kukapambana na Magonjwa Yasiyoambukiza.
Prof. Kambi alisema ametoa msimamo huo kutokana na ukweli kwamba wataalamu wa sekta hiyo wanashughulikia afya ya binadamu kwa hiyo ni lazima wafanye kazi zao kwa kuzingatia weledi na maadili.
“Mtu yeyote ambaye ni mtumishi katika sekta ya afya ni lazima afanye kazi zake kwa kuzingatia weledi na maadili ya taaluma, hivyo ndivyo taaluma zetu kwenye sekta ya afya zinavyotaka” alisema Prof. Kambi na kuongeza kuwa:
“Kwa hiyo mtu ambaye hatafuata weledi na maadili sisi kama Serikali hatutaweza kumvumilia kwa sababu tunashughulikia afya ya binadamu kwa hiyo ni lazima kazi hizi tuzifanye kwa kuzingatia weledi na maadili”
Kuhusu mkutano huo, Mganga Mkuu huyo wa Serikali, aliwaomba washiriki wa mkutano huo kuangalia na kujadili changamoto mbalimbali za taaluma ya Neuroradiolojia ili waisaidie Serikali kupata mawazo na ushauri wa jinsi ya kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo.
Akizungumzia vifaa muhimu katika hospitali za Kanda nchini, Prof. Kambi alisema Serikali inafanya jitihada za kuhakikisha hospitali zote za Kanda angalau zihakikishe zinapata vifaa vya Ultrasound, CT Scan na MRI ambazo ni muhimu katika kutoa huduma za afya.
Aliongeza kuwa hali si mbaya katika vituo vya afya kuhusu masuala ya vipimo kwa sababu hospitali nyingi za Serikali zina vipimo vikubwa muhimu kwa utoaji wa huduma ya afya kwenye hospitali hizo.
“Kwa mfano kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili tuna Ultrasound, tuna CT Scan,  tuna MRI.Ukienda hospitali ya Bugando baadhi ya vipimo vipo vingine havipo, ukienda kwenye Hospitali ya Kanda ya Mbeya nako kuna baadhi vipo na vingine havipo” alisema na kufafanua kuwa:
“Lakini sisi kama Serikali tunafanya jitihada za kuhakikisha hospitali zote za Kanda angalau zihakikishe zinapata vifaa vyote  hivi ambavyo ni muhimu katika kutoa huduma za afya”.
 Kwa upande wake Mkufunzi Muandamizi wa Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili na Mwenyekiti wa Baraza la Walaamu wa Radiolojia Nchini (MRIPC) Dkt. Ramadhani Kazema alisema jukumu la baraza hilo ni kuangalia kama wataalum wa Radiolojia wanakidhi mahitaji katika mafunzo na wanafanya kazi zao kwa weledi.
“Changamoto zinazoikabili tasnia hii katika nchi hasa za Afrika ni uhaba wa fedha na kuna jitihada zimefanywa ili kuboresha upatikanaji wa fedha kama unavyojua bajeti za hospitali ni kidogo ziko finyu kwa hiyo inakua na athari kwenye utendaji wetu wa kazi” alisema Dkt. Kazema.
Alifafanua kuwa pamoja na wataalamu wa Radiolojia kuwa si wa kutosha lakini wanaridhisha na vitendea kazi vipo vinaridhisha ,ingawa changamoto ni jinsi ya kuvifanya vitendea kazi hivyo viendelee kufanya kazi kwa muda wote.
Mkutano huo wa siku mbili wa Wataalamu wa Nuerolojia unajadili Mada kuu inayosema “Jukumu la Neuroradiolojia katika kukabialiana na Magonjwa Yasiyoambukiza na kushirikisha wataalamu kutoka Kenya, Marekani, Uganda, Korea Kusini, Uingereza na Tanzania.
Hata hivyo, mkutano huo pia unatarajia kushirikisha wataalamu hao kubadilishana uzoefu na utaalaamu katika masuala ya Neuroradiolojia na kujadili masuala ya ugonjwa ya kansa ya matiti.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Unyayo wangu ni kipindi kipya kabisa kinachokujia kupita Tone Tv, ambacho kinaletwa kwenu na Mtangazaji wetu Eddie Nyota , kinacholenga shabaha ya watu waliothubutu kufanya jambo fulani katika jamii na wanauelewa na jamii husika. Utajifunza mengina kuburudika pia kupitia kipindi hiki Kinacholenga rika zote.
 

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa