Na Raymond Mushumbusi WHUSM
Watanzania wameaswa kuzingatia umri katika kungalia filamu katika majumba ya sinema na sehemu mbalimbali.
Wito huo
umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu
Tanzania Bibi. Joyce Fisso wakati akifafanua masuala mbalimbali kuhusu
tasnia ya filamu nchini kwa waandishi wa habari.
Bibi
Joyce Fisso amesema kuwa Bodi yake inafanya kazi ya kuzipa kiwango kazi
za filamu na maigizo ikiwemo umri sahihi wa kuangalia filamu na hili
linapaswa kuzingatiwa na waoneshaji na waangaliaji wa Filamu.
“ Natoa
wito kwa watanzania hasa wazazi kuzingatia umri katika kuangalia filamu,
ukiona imeandikwa umri wa miaka 18 ujue ni maalum kwa ajili ya umri huo
na mtoto chini ya hapo hatakiwa kuangalia kwasababu maudhui ya filamu
au maigizo hayo hayamuhusu alisisitiza Bibi. Joyce.
Bibi
Joyce Fisso ameongeza kuwa jukumu la kujenga maadili kwa watanzania hasa
watoto lipo mikononi mwa wazazi wao na kuwaasa wazazi kuzingatia umri
katika kuangali filamu na maigizo mbalimbali ili kupunguza wimbi la
mmomonyoko wa maadili nchini.
Aidha Bibi Joyce Fisso ameshauri waandaaji wa filamu na maigizo nchini kuandaa filamu na maagizo yenye maudhui ya watoto ya
kuwajenga katika Mila, Desturi na Tamaduni za kitanzania kwa kuwa ndio
kizazi cha baadae na kinatakiwa kulelewa katika maadili mema.
Bodi ya
Filamu inapokea filamu na maigizo mbalimbali kwa ajili ya kupata kibali
cha kusambazwa na zaidi ya asilimia 70 ya filamu hizo maudhui yake ni
mapenzi hivyo basi jamii inatahadharishwa
kuzingatia umri uliowekwa katika filamu na maigizo hayo ili kuepukana na
mmomonyoko wa maadili kwa watoto uanaozidi kuongezeka siku hadi siku
kwa kuangalia filamu na maigizo yenye maudhui yasiyowahusu.
0 comments:
Post a Comment