Na: Lilian Lundo – MAELEZO
Waziri
wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amesema
kuwa wanafunzi 290 kati ya wanafunzi 7,805 wa Stashahada Maalum ya
Ualimu Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) waliorejeshwa nyumbani Mei, 2016
kutokana na mgomo wa walimu katika chuo hiko hawakuwa na sifa ya
kujiunga na programu hiyo.
Prof.
Ndalichako aliyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa
ufafanuzi kuhusu maamuzi yaliyochukuliwa na Serikali baada ya
kugundulika kudahiliwa kwa wanafunzi wasiokuwa na sifa katika programu
hiyo.
“Programu
hii ilikuwa maalumu kwa ajili ya kutatua tatizo la upungufu wa walimu
wa sayansi nchini, ambapo wanafunzi waliotakiwa kujiunga na programu hii
ni wale waliomaliza kidato cha nne na wamefaulu Daraja la I hadi la III na kupata alama C au zaidi kwa masomo mawili ya Sayansi na Hisabati,” alifafanua Prof. Ndalichako.
Aliendelea
kwa kusema kuwa, kati ya wanafunzi 290 wasiokuwa na sifa wapo ambao
walidahiliwa pasipokuwa na alama C au zaidi katika masomo ya sayansi na hisabati na wengine ambao walifaulu kwa Daraja la IV kinyume na Sifa zilizotolewa.
Aidha,
Mhe. Ndalichako amesema kuwa programu hiyo ilikuwa maalumu kwa ajili ya
walimu wa Sekondari ili kutatua tatizo la uhaba wa walimu wa Sayansi na
Hisabati katika shule za Sekondari lakini kuna wanafunzi 1,210
waliokuwa wakisoma Stashahada ya Ualimu wa shule ya Msingi kinyume cha
matakwa ya programu hiyo.
Hivyo basi,
Serikali imewarejesha wanafunzi 382 kuendelea na masomo yao chuo kikuu
cha UDOM, wanafunzi wengine 4,586 watahamishiwa vyuo vya ualimu
Morogoro, Butimba, Mpwapwa, Songea na Tukuyu pamoja na wanafunzi 1,337
ambao watahamishiwa kwenye vyuo vya Ualimu Korogwe na Kasulu.
Aidha,
wanafunzi 290 waliokosa sifa wameshauriwa kuomba mafunzo yanayolingana
na sifa walizonazo kwenye vyuo watakavyotaka na wale waliokuwa wakisomea
Ualimu shule ya Msingi 29 watahamishiwa chuo cha Ualimu Kasulu kumalizi
masomo kwa gharama zao na wanafunzi 1,181 wametakiwa kuomba mafunzo
yanayolingana na sifa walizonazo.
Hata
hivyo, Serikali itaendelea kuwapatia mikopo wanafunzi watakaorejeshwa
UDOM na watakaohamishwa kwenye vyuo vya Ualimu vya Serikali watapewa
mkopo wa kiasi cha Sh. 600,000 kwa mwaka ambayo ni ada ya mafunzo ya
Ualimu itakayolipwa moja kwa moja chuoni.
Prof. Ndalichako amesema kuwa mgomo wa walimu wa chuo cha UDOM umetokana na wingi wa
wanafunzi waliodahiliwa kwa ajili ya stashahada maalumu ya ualimu
ambapo wanafunzi 7,845 walidahiliwa huku chuo kikiwa na uwezo wa kuwa na
wanafunzi 1,080.
Walimu
hao, walikuwa wakifundisha wanafunzi wa stashahada ya ualimu na
wanafunzi wa Shahada wa chuoni hapo hali iliyopelekea walimu hao
kuzidiwa wakati huo huo, uongozi wa chuo haukuwa ukitoa fedha za ziada
kwa walimu hao, hivyo kupelekea kugoma kutokana na changamoto walizokuwa
wakikabiliana nazo.
0 comments:
Post a Comment