Home » » CHADEMA yaahirisha maandamano yaliyopangwa kuanza kesho

CHADEMA yaahirisha maandamano yaliyopangwa kuanza kesho


Na Godfriend Mbuya
Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe  ametangaza rasmi , kusitisha maandamano na mikutano ya siasa iliyokuwa ifanyike nchi nzima kuanzia kesho Septemba Mosi ili , kupisha nafasi ya viongozi wa dini kukutana na Rais Dkt. John Magufuli kutafuta suluhu ya kisiasa.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam . Mbowe amesema CHADEMA imefikia uamuzi huo muhimu baada ya vikao na wito kutoka kwa viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali pamoja na asasi za kiraia.

“Viongozi wa dini na asasi za kiraia wametuomba, tusitishe maandamano hayo ili wapate nafasi ya wiki tatu mwezi huu kukutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli ili kutafuta suluhu ya kisiasa na kama ikishindikana Octoba Mosi maandamano hayo yataratibiwa upya” Amesema Mbowe

Aidha Mbowe amewataka wanachadema na wafuasi wa chama hicho kuwa watulivu wakati wakisubiri viongozi wa dini kufanya mazungumzo hayo ili haki yao ya kikatiba iweze kupatikana.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa