Na Godfriend Mbuya
Waziri
wa nchi ofisi ya rais TAMISEMI George Simbachawene amesema halmashauri
na mikoa nchini imepiga hatua kubwa katika kusimamia na kutekeleza
miradi ya maendeleo ikilinganishawa na miaka ya nyuma.
Akizungumza
na kipindi cha East Africa BreakFast cha East Africa Radio , Waziri
Simbachawene amesema kwa sasa hali imeanza kuridhisha katika nidhamu ya
matumizi ya fedha za umma na usimamiaji wa miradi ya maendeleo, jambo
ambalo linatia moyo katika utendaji wa serikali.
“Hali
inaendelea vizuri na kwa kweli kama tukiendelea hivi, kusimamia miradi
ya maendeleo na ukusanyaji wa mapato ya ndani kama tulivyoanza Januari
hadi sasa tutapiga hatua kubwa sana katika halimashauri zetu”
Kila
fedha ambayo imepelekwa unaiona inapelekwa kwenye maendeleo inatumika
kama ilivyokusudiwa na tabia ya kusimamiana imeonyesha kwamba ndani ya
muda mfupi wananchi wataanza kufurahia miradi mbalimbali inayotekelezwa
sehemu mbalimbali.
Aidha
Waziri amesisitiza kwamba mabadiliko ya kizalendo yana dalili ya
kufungua Tanzania mpya yenye watu waadilifu na taifa lenye kufuata
sheria na utaratibu.
0 comments:
Post a Comment