Home » » Taasisi za umma kuwekewa mita za maji- Lwenge

Taasisi za umma kuwekewa mita za maji- Lwenge


Na Godfriend Mbuya
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge amesema taasisi za umma zitawekewa mita za maji ili kuwezesha kukusanya mapato yatakayosaidia mamlaka za maji nchini kuweza kujiendesha.
Akizungumza Mkoani Mtwara Mhandisi Lwenge amesema amefikia uamuzi huo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa Mamlaka ya Maji safi na maji taka mkoani Mtwara (MTUWASA) kuhusu deni la maji ambalo wanadai taasisi za serikali  ambapo kiasi cha milioni 800 jambo ambalo ni kikwazo katika kuendeleza shughuli za kuwahudumia wananchi.
“Baaada ya kupata malalamiko haya inabidi sasa taasisi za umma ziwekewe mita ili kuweza kuchangia huduma ya maji na kwa kufanya hivyo mamlaka zitaweza kujiendesha katika kupeleka huduma na kutatua baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo”Amesema Lwenge
Aidha baadhi ya wananchi mkoani Mtwara wamelalamikia kuchangia huduma ya maji lakini maji yenyewe hawayapati kama ipasavyo.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa