Na Sheila Simba,MAELEZO
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George
Simbachawene amesema kuwa Rais Magufuli amedhamiria kuwatumikia
wananchi na kuhakikisha maendeleo yapatikani kwa Watanzania wote.
Akizungumza
katika kipindi kipya cha "TUNATEKELEZA" kinachoandaliwa na Idara ya
Habari-MAELEZO na TBC1 Waziri Simbachawene alisema kuwa serikali ipo kwa
ajili ya kufanya kazi ya kuwatumikia wananchi katika kila sekta ili
kutatua changamoto zinazowakabili.
“Kupitia
falsafa yetu ya hapa kazi tu tutahakikisha tunawaletea wananchi
maendeleo kutokana na ahadi zilizoaidiwa kutoka katika ilani 2015-2020
ya Chama Cha Mapinduzi kilicho na serikali.”
Alisisitiza
kuwa Rais Magufuli ameamua kuleta mabadiliko ya kweli hapa nchini
ambayo yanalenga kuwabana wabadhirifu wa mali za umma na kurejesha
kurejesha nidhamu ya kazini jambo ambalo limeanza kuonekana katika Ofisi
mbalimbali za umma.
Waziri
huyo amewahakikishia wananchi kuwa ahadi za maendeleo zilizotolewa na
Serikali ya awamu ya tano zitatekelezwa kama ilivyopangwa kwani wanayo
dhamira ya kweli ya kuwatumikia wananchi.
Alisema
kuwa suala la kusimamiana kazini ni la kawaida na ni wajibu wa kila
mtumishi hakikishe anatimiza wajibu wake katika nafasi aliyopewa ili
aweze kutekeleza majukumu yake kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi wa
serikali kwa kuweka uzalendo mbele.
Aliongeza
kuwa ari na nidhamu ya utendaji kazi mikoani imebadilika na watu
wanafanya kazi kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora,kwani baadhi ya
watumishi wa Halmashauri walikuwa wanafanya kazi kwa mazoea.
Kuhusu
watumishi hewa alisema kuwa serikali imeondoa watumishi 12,000 waliokua
wananchukua mishahara bila kufanya kazi na kuomba wananchi kuunga mkono
juhudi za serikali katika hatua wanazochukua.
“upangaji
mzuri wa watumishi kwenye maeneo ya utoaji huduma kwa wananchi kwa
maana ya Halmashauri utakuwa umekaa vizuri kwa asalimia kubwa hata kwa
kuwapanga vizuri bila wafanyakazi hewa kuwepo”alifafanua Waziri
Simbachawene
Alisema
kuwa suala la wataalamu wa fani mbalimbali kupendelea kubaki mijini ni
tabia na kukosa uzalendo kwani baadhi ya watumishi wanaopagiwa mikoani
hawaripoti kutokana na mazingira jambo ambalo sio sahihi.
“hata
huku mijini wanakokimbilia hakuna nyumba za watumishi basi imekuwa ni
tabia tu ya watu kukosa uzalendo”alisema Simbachawene.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment