Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Makundi 6 kutoana jasho Fainali za Dance100% Jijini DSM

Makundi 6 kutoana jasho Fainali za Dance100% Jijini DSM




Na Godfriend Mbuya



Kesho Jumamosi Septemba 24 ni Fainali za Shindano la Dance100% linaloendeshwa na EATV, ambapo fainali zitafanyika katika viwanja vya Don Bosco Osterbay Jijini Dar es salaam kuanzia saa sita mchana.



Akizungumza kuhusu maandalizi ya shindano hilo Mratibu Bhoke Egna amesema , mambo yote yanayohusu shindano yamekamilika ambapo mshindi wa kwanza ataibuka na kitita cha shilingi milioni 7.



“Maandalizi yamekamilika ambapo mshindi wa kwanza ataibuka na milioni 7 na tunatarajia kuwa na Jaji mpya atakayeshirikiana na majaji wengine ambapo Msanii wa Bongo Flava Ali Kiba atashiriki kazi hiyo” Amesema Bhoke.



Kwa upande wake Jaji wa shindano hilo Super Nyamwela amesema , majaji wameweza kuwatembelea washiriki wa shindano hilo na kuwaelekeza mambo ya msingi ya kuzingatia.



“Tumewaelekeza mambo ya kuzingatia na kwa kweli wamejiandaa vizuri na fainali zitakuwa na ushindani wa hali ya juu sana hivyo tunawaalika wananchi wote kuja kwa wingi kutizama vipaji vya wasanii hawa” Amesema Nyamwela.



Shindano la Dance100% 2016 kesho linafikia tamati kwa mwaka huu ambapo shindano limedhaminiwa na Vodacom kwa kushirikiana na Coca – Cola , na matukio yote yataonyeshwa na EATV siku ya Jumapili saa moja jioni.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa