Na Godfriend Mbuya
Shirika la ndege la Precision Air, limerudisha rasmi safari zake
za kuelekea HAHAYA nchini Comoro kuanzia leo tarehe 27 Septemba 2016.
Ndege kuelekea Comoro iliondoka saa 4 asubuhi kuelkea HAHAYA na
ilitarajiwa kuwasili huko saa 5 Asubuhi. Precision Air ilisitisha safari hizo
mnamo mwaka 2014 na kutangaza kuzirejesha mapema mwezi Agosti mwaka huu.
Akizungumzia kurejeshwa kwa safari hizo Mkurugenzi wa biashara wa
shirika hilo Robert Owusu amesema
kuwa Precision Air imejipanga kutoa
huduma ya uhakika ya usafiri wa anga kati ya Tanzania na Comoro, ambayo
itarahisisha biashara na safari kati ya nchi hizo.
“Safari zetu zitakua kila siku ya Jumanne, Alhamisi na Jumamosi ratiba hii imepangwa mahususi kukidhi
mahitaji ya safari za kiserekali, kibiashara na hata zile za mapumziko na kulingana na mapokeo ya soko tunatarajia
kuongeza safari zaidi.” Amesema Owusu amedokeza.
“Tunafuraha kurudisha
safari hizi kama tulivyo ahidi , na hii itakua sehemu ya 13 katika mtandao wetu
kwa ujumla na ni ya pili kwa safari zetu za kikanda.
Nimatazamio yetu
kutengeneza mtandao wa safari ambao utawawezesha abiria wetu kuunganisha safari
zao ndani ya Afrika Mashariki, Africa na Duniani kwa ujumla. Tunajivunia kuwa
na mtandao bora ziaidi unaowapa wateja urahisi wa kuunganisha safari zao na
hatutachoka kuuboresha kuhakikisha tunaendana na matakwa ya soko.”
Amesisitiza Owusu.
Precision air ndilo shirika
pekee la Kitanzania lilo chini ya umoja wa Mashirika ya Ndege Duniani IATA na
hivyo huwawezesha abiria kufanya booking zao na kuunganisha na mashirika
mengine ya Kimataifa.
Aidha kwa safari za ndani
Precision Air inasafiri kwenda sehemu 13 ikitokea Dar es Salaam kuelekea Arusha,
Kilimanjaro, Mwanza, Bukoba, Musoma, Tabora, Kigoma, Mtwara, Zanzibar and
Pemba.
0 comments:
Post a Comment