Na Raymond Mushumbusi WHUSM.
Serikali
ya Tanzania na Iran zakubaliana kuanzishwa kwa wiki ya Utamaduni
itakayowezesha kujifunza namna ya kuukuza ,kuulinda na kuendeleza sekta
hiyo.
Makubaliano
hayo yamebainishwa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipokutana na Naibu
Waziri wa Utamaduni kutoka Iran Mhe. Abuzar Ebrahimi Turkaman kujadili
masuala ya ushirikiano katika sekta ya Utamaduni kati ya Tanzania na
Iran.
Waziri Nnauye alisema kuwa amekubaliana na wazo la kuanzishwa kwa wiki ya Utamaduni kati ya Tanzania na Iran ni fursa pekee ya kujifunza kutoka kwao namna ya kuukuza, kuulinda na kuuendeleza utamaduni wa mtanzania.
“Utamaduni
ni silaha ya upendo na nimefurahia wazo la kuanzisha wiki ya Utamaduni
na tuko tayari kujifunza kutoka kwenu na hakika tumelipokea na tunaamini
fursa hii italeta mafanikio makubwa katika sekta hii”, alisema Mhe.
Nnauye.
Kwa
upande wa Naibu Waziri wa Utamaduni Iran Mhe. Abuzar Ebrahimi Turkaman
aliihakikishia Serikali ya Tanzania kuwa wataendelea kushirikiana katika
masuala ya Utamaduni na kuendelea kujifunza kutoka kwa watanzania namna
bora ya kuuenzi,kuuendeleza na kuutunza Utamaduni.
Naibu
Waziri huyo wa Iran aliendelea kusema serikali yake iko tayari
kushirikiana na Tanzania katika uandaaji wa Filamu na kubadilishana
uzoefu katika masuala ya filamu kati ya nchi hizo mbili.
Hata hivyo Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nnauye alipata mwaliko kutoka kwa Naibu Waziri wa Utamaduni Iran Mhe. Turkaman kwenda nchini Iran kujionea vivutio vya Utamaduni.
0 comments:
Post a Comment