Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Vodacom yaitaka Simba na Yanga kutoa burudani Jumamosi

Vodacom yaitaka Simba na Yanga kutoa burudani Jumamosi


Kampuni ya Vodacom imezitaka klabu za Simba na Yanga kuwaburudisha watanzania katika mchezo wa Jumamosi hii katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam
Akizungumza na EATV Jijini Dar es salaam kwa niaba ya Vodacom Tanzania ambao ni wadhamini wa Ligi Kuu ya Tanzania bara, Mkuu wa Kitengocha Masoko cha Masoko na Mawasilino, Nandi Mwiyombella amesema wakiwa kama Vodacom wanazitakia kila la kheri timu za Simba na Yanga katika mchezo wa Jumamosi Octoba Mosi 2016.
“Simba na Yanga zinapambana katika mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara Jumamosi hii, sisi kama Vodacom na wadhamini wakuu wa ligi hii tunawatakia kila la heri na tunaamini kwamba mchezo wao utakuwa ni burudani tosha kwa mashabiki wa soka hapa nchini” Amesema Nandi.
Nandi ameongeza kuwa Vodacom inaamini kwamba mchezo huo utakuwa mzuri na wakuburudisha na inawaondoa hofu mashabiki wote ambao watafika uwanjani kwani ni mara ya kwanza kwa msimu huu kwamba watafurahia viwango vitakavyooyeshwa na pande zote mbili.
Aidha mashabiki ambao hawatafanikiwa kufika uwanjani wanaweza kupata matokeo hayo ‘live’ kwa kujiunga na kifurushi cha ‘soka bando’ kifurushi ambacho kinapatikana kwa shilingi 500 na kinatoa fursa kwa wanamichezo kupata matokeo ya mechi kati ya Simba na Yanga na ni kifurushi kwa ajili ya mashabiki wa soka ambapo unaweza kupata matokeo ya mechi popote pale ulipo na dakika 14 za kupiga Vodacom Kwenda Vodacom na dakika 2 kwenda mitandao mingine pia utapata sms 20 kwa masaa 24.

,Pia napenda kuwatoa wasiwasi wapenzi wa mchezo huu ambao hawatapata na nafasi ya kufika uwanjani kwani Vodacom Tanzania haitawaacha mbali na
Ili kununua kifurushi hiki anachotakiwa kufanya mteja ni kupiga  namba *149 * 01#, Ofa mpya alafu chagua ‘Soka Bando’. Baada ya  hapo mteja atapata ujumbe unaomtaka ajisajili kwa timu ya soka anayoishabikia kwa kutuma jina la timu mfano “Yanga”  “Simba” au “Azam” nk. kwenda namba 15460


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa