Na Beatrice Lyimo
MAELEZO
Dar es Salaam
27.10.2016.
SERIKALI
imeahidi kuendeleza uhusiano na ushirikiano na vyombo vya habari nchini
ili kuviwezesha kutelekeleza vyema wajibu wake kwa umma.
Akizungumza
katika wakati tofauti wakati wa ziara yake ya kutembelea taasisi za
Vyombo vya habari leo Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Habari Hassan
Abbas alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa vyombo vya habari
vinakuwa chachu ya maendeleo ya wananchi nchini.
Aliongeza
kuwa yapo mafanikio mbalimbali yaliyofikiwa na Serikali katika sekta
mbalimbali nchini ikiwemo umeme, maji, barabara, afya, elimu, ambapo
taarifa za utekelezaji wa ahadi hizo za Serikali hazijaweza kuandikwa na
kutangazwa na vyombo vya habari.
Abbas
alisema katika kuimarisha mfumo wa utoaji wa habari na taarifa kwa
umma, ofisi yake kwa kushirikiana na Shirika la Utangazaji nchini (TBC)
wameanzisha kipindi cha TUNATEKELEZA ambacho kinatoa fursa kwa Viongozi wa Serikali kutoa taarifa kwa umma kuhusu utelekezaji wa mipango mbalimbali ya Serikali.
Aidha
Abbasalisema ofisi yake ndiye msimamizi na mratibu mkuu wa vitengo vya
mawasiliano Serikali, hivyo alitoa wito kwa wanahabari kuwasiliana naye
mara kwa mara pindi wanapokabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo
upatikanaji wa taarifa katika ofisi za umma.
Kuhusu
mafunzo kwa wanahabari, Abbas alivitaka vyombo vya habari kutumia fursa
ya waandishi wakongwe waliopo katika ofisi zao, ambao wamebobea katika
maeneo mbalimbaloi ikiwemo uandishi wa makala, habari na upigaji picha.
Kwa
mujibu wa Abbas alisema kwa sasa, ofisi yake inaendelea na zoezi la
kuwahamasisha Maafisa Habari wa Serikali katika Wizara, Idara, Taasisi,
Wakala, Mikoa, na Wilaya nchini kuanza mageuzi katika mfumo wa taarifa
kwa umma ikiwemo kutumia mitandao ya kijamii.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment