Home » » BARAZA LA WAFANYAKAZI LITUMIKE KUTATUA MIGOGORO YA WAFANYAKAZI – MAKAMBA

BARAZA LA WAFANYAKAZI LITUMIKE KUTATUA MIGOGORO YA WAFANYAKAZI – MAKAMBA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



NA EVELYN MKOKOI  - DSM

Tawi la baraza la wafanyakazi katika Ofisi ya makamu wa Rais limetakiwa kuwa ndo sehemu sahihi ya kujadili na kutatua migogoro ya wafanyaki na siyo majukwaa ya siasa.
Hayo yameelezwa leo na Waziri wa Nchi anayeshughulikia masuala ya Muungano na Mazingira Mhe January Mkamba, Lipokuwa akizungumza na wajumbe wa Baraza la wafanyakazi katika Ofisi ya Makamu wa Rais Mtaa wa Luthuli jijini dar  es Salaam.
 Mhe.Makamba alisema kuwa vikao vya baraza la wafanyakazi vimekuwepo kisheria na ni muhimu wajumbe kukaa pamoja kujadili masuala ya msingi yanyowahusu watumishi kwani wao ndo waliowachangua hivyo, majadiliano yanayokuwepo  katika vikao hivyo ni nyenzo muhimu ya kuondoa migogoro na migomo mahala pa kazi.
.
“Nyie ni miongoni mwa watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais ambao kwa namna moja au nyingine mmeaminiwa na kukabidhiwa dhamana ya kuwawakilisha wenzenu katika chombo hiki muhimu, katika kuamua na kushauri Baraza juu ya masuala mbalimbali yanayolenga kuleta ufanisi na utulivu ndani ya Ofisi yetu.alisisita Makamba”.


Aidha, Waziri Makamba alisema kwamba, Lengo la vikao vya Baraza ni kuleta ufanisi wa utendaji kazi mahala pa kazi kwa ajili ya manufaa ya Taifa  kuelekezana, kushauriana na kukumbushana, kuhusu majukumu ya ofisi  na ushiriki wa wafanyakazi katika kuyatekeleza na kuyasimamia, na aliongeza kwa kusema kuwa  ni fursa ya kipekee ya kutafakari utendaji wa kazi na majukumu ya Ofisi kwa ujumla.
Kikao hicho cha baraza la wafanyakazi cha Ofisi ya makamu wa Rais kimudhuriwa na wawakilishi kutoka TUGHE Taifa na Mkoa na Wawakilishi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Zanzibar.


0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa