Home » » NAIBU WAZIRI WA AFYA DKT. HAMIS KIGWANGALLA AMWAGIZA MKEMIA MKUU KUFANYA UCHUNGUZI WA KIMAABARA WA VILAINISHI.

NAIBU WAZIRI WA AFYA DKT. HAMIS KIGWANGALLA AMWAGIZA MKEMIA MKUU KUFANYA UCHUNGUZI WA KIMAABARA WA VILAINISHI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na Ally Daud

MAELEZO

Dar es Salaam.

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mh. Dkt. Hamisi Kigwangalla amemuagiza Mkemia Mkuu wa Serikali Prof. Samwel  Manyele kuendelea na uchunguzi wa kimaabara kwa vilainishi vilivyo sokoni ili kubaini bidhaa isiyokidhi viwango.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam wake na Dkt. Kigwangalla amesema Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali haina budi kuendeleza uchunguzi wa kimaabara ili kubaini vilainishi visivyo na viwango na ubora ambavyo vinaendelea kutumiwa.

“Tunapiga marufuku uuzaji wa vilainishi vya kupima unaofanyika mtaani na sokoni kwa sababu vifungashio vya vilainishi hivyo havikidhi ubora” alisema Dkt. Kigwangalla.

Aidha Dkt. Kigwangalla amesema Serikali itaendelea kupiga marufuku kuingizwa kwa vilainishi vilivyotumika (recycled lubricants) visivyo na ubora na visivyo kidhi  matakwa ya kisheria kwani vinachangia uharibifu wa vyombo vya moto nchini.

Kwa mujibu wa Dkt. Kigwangalla amesema kuwa asilimia 50 ya vilainishi vya injini, aina ya petroli zilizochunguzwa zilionekana kutokikidhi viwango vya ubora vya vilainishi vya kitaifa.

Kwa upande wake Mkemia Mkuu wa Serikali, Prof. Samwel Manyele amesema kuwa amepokea agizo la Naibu Waziri na amesema kuwa  uchunguzi wa kimaabara wa sampuli za vilainishi zinazoingizwa nchini unafanyika na kuendelea.

Aidha Prof. Manyele amesema kuwa mpaka sasa wamesajili  kampuni 28 za kuingiza vilainishi nchini na wameimarisha  ukaguzi wa mizigo ya vilainishi katika viwanda, bandari, bandari kavu, mipaka na viwanja vya ndege.

Kwa mujibu wa Prof. Manyele amesema kuwa miongoni mwa vilainishi hivyo vinavyoingia nchini ni pamoja na mafuta ya kulainishia injini ,Diseli na Petroli

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa