Na Ally Daud-MAELEZO
Serikali imeendelea kukanusha taarifa
za uwepo wa ugonjwa wa zika nchini kuafuatia uwepo wa taarifa za ugonjwa huo
zilizosambaa mwishoni wa wiki hii.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa
kampeni ya kufanya mazoezi uliofanyika leo jijini Dar es salaam Mganga Mkuu wa
Serikali Prof. Mohammed Kambi amesema kuwa hakuna ugonjwa wa zika wala mtu
aliyethibitishwa kuwa na virusi vya ugonjwa huo.
“Ule ulikua utafiti wa awali wa kujaribu kipimo cha kupima
ugonjwa wa zika na si vinginevyo kama taarifa zilivyoenea hivi karibuni
nchini”alisema Prof. Kambi.
Aidha Dkt. Kambi amesema kuwa
Watanzania waondoe wasiwasi ila wajikinge zaidi ili kuepuka kabisa ugonjwa huo
usiingie nchini kwa ajili kujenga taifa lenye wananchi wenye afya imara.
Mwisho.
0 comments:
Post a Comment