Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » MAADHIMISHO YA MIAKA 10 YA KAMPUNI YA MAGAZETI YA SERIKALI (TSN)

MAADHIMISHO YA MIAKA 10 YA KAMPUNI YA MAGAZETI YA SERIKALI (TSN)

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (kushoto) akiwa ameongozana na Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Dkt. Jim Yonaz wakielekea katika ukumbi ambako hafla ya Miaka 10 ya Kampuni hiyo ikifanyika leo 26/01/2017 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akiongea na Wafanyakazi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) wakati wa hafla ya Miaka 10 ya Kampuni hiyo iliyofanyika leo 26/01/2017 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya Wafanyakazi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) wakimsikiliza Waziri Nape Nnauye wakati alipokutana nao kwenye Maadhimisho ya Miaka 10 ya Kampuni hiyo leo 26/01/2017 jijini Dar es Salaam.

Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Dkt. Jim Yonaz akiongea na wageni waalikwa pamoja na wafanyakazi wa Kampuni hiyo wakati wa hafla ya Miaka 10 ya Kampuni hiyo iliyofanyika leo 26/01/2017 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.





Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye(wa tatu kushoto) pamoja Viongozi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali na Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) wakikata keki wakati wa hafla ya Miaka 10 ya Kampuni hiyo iliyofanyika leo 26/01/2017 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (kulia) akiteta jambo na Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Dkt. Jim Yonaz
wakati wa hafla ya Miaka 10 ya Kampuni hiyo iliyofanyika leo 26/01/2017 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (kulia) akifurahia zawadi ya picha aliyopewa na Kaimu Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Serikali (TSN) Bibi. Tuma Abdallah wakati wa hafla ya kutimiza Miaka 10 ya Kampuni hiyo.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akicharaza gitaa wakati wa hafla ya kutimiza Miaka 10 ya Kampuni hiyo iliyofanyika leo 26/01/2017 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
(Picha zote na Benedict Liwenga-WHUSM)

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa