Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye akimfafanulia sheria
mbalimbali ambazo mfanyabishara wa kazi za filamu na muziki anastahiki
kuzifuata kabla ya kuanza kufanya biashara hiyo. Anaemsikiliaza Mheshimiwa Nape
ni mmiliki wa ghala ambalo shehena kubwa ya kazi haramu za filamu na muziki
zimekamatwa wakati wa operesheni iliyofanyika leo eneo la Kariakoo jijini
Dar-es-Salaam.
Fundi
wa kuchoma vyuma kwa kutumia teknolojia ya gesi akiendelea na zoezi la kuchoma
kufuli ya lango la ghala lililofichwa kwenye hoteli ya Butterfly iliyopo mtaa
wa Muhonda eneo la Kariakoo. Ghala hilo limekutwa na shehena kubwa ya kazi
haramu za muziki na filamu.(P ICHA NA MAELEZO)
Mmiliki
wa ghala lilolokutwa chini ya hoteli ya Butterfly Phili Ulaya akijaribu
kujitetea mbele za Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye
mara baada ya zoezi la kuvunja kufuli ya lango la ghala hilo kukamilika. Waziri
Nape kwa kushirikiana na viongozi wa taasisi zinazosimamia maslahi ya kazi za
ubunifu wamefanya operesheni iliyofanikisha kukamtwa kwa shehema kubwa ya kazi haramu za filamu na
muziki kwenye ghala la bwana Ulaya liliofichwa chini ya hoteli ya Butterfly.
Jengo
la hoteli ya butterfly iliyopo mtaa wa Muhonda, Kariakoo ambalo ghala lenye
shehena kubwa ya kazi za haramu za filamu na muziki zilikamatwa kwenye zoezi
lililoongozwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye.
0 comments:
Post a Comment