Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Profesa Mohamed Janabi akizungumza na wataalamu wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya manunuzi ya Umma kwa watumishi wa tasisi hiyo.
Washiriki wa mafunzo hayo wakisikiliza na kufatilia hotuba ya ufunguzi .
Wataalamu kutoka bodi ya manunuzi na ugavi (PSPTB) wakiongozwa na afisa habari, Shamim Mdee katika mkutano huo .
Mratibu mkuu wa Utafiti na ushauri wa PSPTB, Amos Kazinza akitoa elimu juu ya masuala ya manunuzi kwa watumishi wa tasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete.
Nae Mratibu Mkuu wa utafiti na ushauri wa PSPTB bwana Amos Kazinza, amesama kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2016/17 budget ya serikali imetenga asilimia 76 kwa ajiliya Ununuzi. Hivyo manunuzi huchukua kiasi kikubwa cha fedha. Amesema mabadiliko ya sheria yamelenga kuongeza ufanisi na kuhakikisha kwamba thamani ya fedha inapatikana.
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Profesa Mohamed
Janabi ameshauri juu ya kuwepo kwa sheria ya manunuzi kwa njia ya
mtandao ili kuokoa muda unaotokana na kuzunguka kwa makaratasi katika
ofisi.
Profesa
Janabi ameyasema hayo leo wakati akifungua mafunzo ya watumishi wa
taasisi hiyo wanaohusika na manunuzi ambayo yameratibiwa na Bodi ya
Manunuzi na Ugavi (PSPTB), amesema uwepo wa mafunzo hayo, utasaidia
kutatua changamoto hizo.
"kuendesha
manunuzi katika mtandao kutapunguza gharama ambazo zinaweza kuokoa
fedha nyingi zitakazotumika katika masuala mengine" alisema Profesa
Janabi.
Nae Mratibu Mkuu wa utafiti na ushauri wa PSPTB bwana Amos Kazinza, amesama kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2016/17 budget ya serikali imetenga asilimia 76 kwa ajiliya Ununuzi. Hivyo manunuzi huchukua kiasi kikubwa cha fedha. Amesema mabadiliko ya sheria yamelenga kuongeza ufanisi na kuhakikisha kwamba thamani ya fedha inapatikana.
0 comments:
Post a Comment