Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Ijumaa ya
tarehe 27 januari mida ya jioni, makampuni na mashirika makubwa na madogo pamoja na wafanya biashara mbali mbali
Tanzania walikusanyika katika hotel ya
Hyatt Regency jijini Dar es Salaam kushuudia utowaji wa tuzo za Tanzania Leadership Awards 2016. Tuzo hizi
za heshima hutolewa kwa biashara na wafanyabiashara bora nchini.
Katika
hafla hiyo, ZoomTanzania, tovuti inayoongoza kwa matangazo ya biashara (kununua
na kuuza) nchini, ilinyakuwa tuza ya '
tovuti bora ya mwaka'. Hii ni mara ya pili kwa Kampuni hii ya kitanzania kupewa
heshima kwa utaalamu wake wa mtandaoni, mwaka jana ilishinda tuzo ya kampuni
bora ya biashara za mtandaoni.
Kutokuwa na uwepo wa biashara yako
mtandaoni ni hatari kwa biashara yako
Kuna
watumiaji wa internet zaidi ya milioni 17 nchini Tanzania, wafanya biashara
zaidi na zaidi wanaanza kutambua umuhimu
wa kuwa na uwepo mtandaoni, wengi wao wameanzisha tovuti zao ili kuweza kwenda sambamba na soko
la mtandaoni linalokuwa kwa kasi
Hata
hivyo, wengi wa wafanyabiashara hawana ufanisi wa kubadilisha watumiaji wa
mitandao kuwa wateja.
Kwa bahati
nzuri, kampuni ya ZoomTanzania inaelewa jinsi ya kutengeneza tovuti nzuri ya
biashara itayowavutia watanzania , kwa
leo watakujuza dondoo 5 zitazo kusaidia kuboresha tovuti yako ya biashara mwaka
huu.
1. Ni muhimu tovuti yako itumike
kirahisi kwa kutumia simu za mikononi
Zaidi ya
67% ya Watanzania wanatumia simu za mikononi, na karibu 50% ya watumiaji wa
internet hutumia simu zao kutafuta vitu mtandaoni . Kwa hivyo, kuwa na tovuti
inayotumika kirahisi kwa kutumia simu za mikononi ni muhimu sana ili kupata
wateja wanao tafuta vitu mtandaoni kutupitia simu zao
Kumbuka,
kadri unavyo rahisisha upatikanaji wa tovuti yako ndivyo unavyoweza kubadilisha
watumiaji kuwa wateja
2. Kurasa za tovuti yako zinapaswa
kutoa ufumbuzi
Kama ni mgahawa au kampuni ya ulinzi, watu wanatembelea tovuti yako kwa sababu
wanatafuta ufumbuzi. Hii ina maana kwamba, tovuti yako lazima iweke wazi jinsi
biashara yako itawasaidia kutatua matatizo yao.
Hivyo,
badala ya kusifia biashara yako,
unapaswa kutambua na kuzingatia
changamoto za wateja wako na kueleza jinsi gani unaweza kuwasaidia.
Kwa mfano,
kama kampuni yako inatoa Huduma za matangazo ,basi Kurasa zako zisielezee tu
jinsi gani Huduma zako ndio bora kuliko zingine zote badala yake, ni muhimu
kuwajulisha wateja wako ni faida gani watapata kutangaza kupitia kampuni yako,
kwa mfano ni idadi ya watu wangapi wataona matagazo yao.
3. Ni muhimu kufanya content
marketing
Njia
nyingine ya kutatua matatizo ya watumiaji wako na kuonyesha thamani yako na
uaminifu kama biashara ni kuonyesha kwamba wewe ni mtaalam katika sekta yako.
Njia moja kubwa ya kufanya hivyo ni kuwa na blog kwenye tovuti yako ambayo hutoa taarifa muhimu juu ya mada
ambazo ni muhimu kwa wateja wako.
Aidha, Njia za utafutaji kama Google uzingatia
content marketing hivyo kufanya tovuti yako ionekane juu endapo mteja atakuwa anatafuta kitu katika sekta yako ya biashara ,
Hivyo, kwa
mfano, kampuni ya vifaa vya ujenzi ambayo ina blog na makala kama 'Jinsi ya
Kujenga Nyumba yako mwenyewe', 'Maswali 10 ya kumuuliza Mkandarasi kabla
yakumuajiri ', na' Faida na hasara za kuagiza vifaa vya ujenzi kutoka nje '
itakuwa na uwezekano mkubwa kuonekena kwenye google search pale mtumiaji
anapotafuta tovuti za sekta ya ujenzi
Bado
hujaamini? Utafiti uliofanywa na Hubspot
ulionyesha kuwa biashara ambazo uweka kipaumbele matumizi ya blog
hufurahia mara 13 zaidi ROI kuliko wafanyabiashara ambao hawana blog!
4. Tumia lugha inayofahamika vizuri
na wateja wako
Kiswahili
ni lugha maarufu zaidi katika mazingira rasmi na yasio rasmi nchini Tanzania,
hata hivyo, kwa baadhi ya biashara na
sekta ni muhimu kuwasiliana kwa Kiingereza.
Kama we ni
mfanya biashara wa sekta kama hii ni muhimu
kuwa na tovuti ya lugha mbili (Kiingereza na Kiswahili). Hii itakufanya
uweze kufanya vizuri katika sekta yako inayotumia kiingereza na pia kuvutia
watumiaji wa lugha ya kiswahili wanaotafuta huduma.
5.Tengeneza kurasa zitazo badilisha
watumiaji kuwa wateja
Mwisho wa
siku, lengo kuu la tovuti yako ni kupata wateja. Hivyo, iwe ni jinsi gani
yakuwasiliana na biashara yako, kuweka apointimenti, au kujiunga na blog
ya biashara yako, kila ukurasa inapaswa
kuwa na wito wa kuchukua hatua( call-to-action). Hii ni pamoja na:
• Fomu za kujiunga ( sign up and subscribe )
• Namba za simu na barua pepe kurahisisha
mawasiliano
• Tovuti iunganishwe na mitandao ya kijamii
• Actionable buttons za kurahisisha kupakua materials
za sales na fomu za matangazo
Mtumiaji
hapaswi kupata shida kutafuta kitu katika tovuti yako. Jaribu kurahisisha na
kuweka mambo wazo kadri uwezavyo
Pata matokeo unayoyataka
Kadri idadi ya watumiaji wa internet inavyoendelea
kuongezeka nchini Tanzania, ndivyo watu zaidi na zaidi wavyozidi kutafuta
bidhaa na huduma mtandaoni. Kwa bahati nzuri, dondoo hizi 5
zitarahisisha tovuti yako ipatikane kirahisi, kufanya wateja wengi watumie tovuti yako na
kufanya biashara yako iwe juu zaidi ya washindani wako.
Kama unataka biashara yako ionekane
zaidi mtandaoni, Jifunze zaidi kuhusu ufumbuzi wa matangazo toka ZoomTanzania bofya hapa.
0 comments:
Post a Comment