Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Mshindi wa Tigo Reach for Change kutangazwa March 9

Mshindi wa Tigo Reach for Change kutangazwa March 9

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Washiriki Wa Tigo Reach  For Change Waliofanikiwa Kuingia Katika Mchujo Wa Mwisho Wakiwasilisha Wazo Lao Ubunifu Mbele Ya Majaji Mapema Wiki Hii Katika Ofisi Za Makao Makuu Ya  Tigo ,Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam.



Majaji wa Tigo Reach for Change wakimsikliza kwa makini mmoja wa washiriki aliyefanikiwa kuingia katika mchujo 




Na Mwandishi Wetu

  Mashindano ya mwaka huu  ya Waleta mabadiliko ya kidijitali wa Tigo yamefikia katika hatua ya juu  ya kuchagua washindani watano  kufuatia mchakato wa mapitio ambao ulijumuisha waombaji 358. Shindano hili hufanyika kila mwaka na liko wazi  kwa waombaji kutoka  nchi nzima  limejielekeza katika  kuibua vijana mahiri  walio na ubunifu wa miradi ya kidijitali inayoboresha maisha ya watu, hususani watoto kwa kutumia programu za kidijitali.

  Vijana watano wanaoingia katika hatua ya fainali  hupata nafasi ya kuhudhuria warsha  ya maendeleo ya maudhui ya siku mbili pamoja na kuwasilisha miradi yao wakisubiri uthibitisho wa mwisho  kutoka kwa jopo la wataalamu wa ndani na nje katika ujasiriamali na stadi za  kidijitali.

  Waleta mabadiliko  wa Kidijitali wa Tigo ni wazo  la Kampuni ya Tigo kwa kushirikiana na asasi isiyo ya kiserikali ya Reach-for- Change ikiwa ni programu ya ushauri na  kuunga mkono  ambayo inawapa washindi fursa ya kuanzisha ujasiriamali endelevu katika maeneo ya elimu,  ujumuishwaji wa kidijitali na shughuli za ujasiriamali.

  Meneja wa Huduma za kijamii wa Tigo, Halima Okash alisema kuwa  washindi wawili wa kwanza  watapata  fedha taslimu dola 20,000 (takribani shilingi milioni 44,000,000) kuwezesha utekelezaji wa maudhui yao.


  “Miradi hii ina matokeo makubwa kijamii, inatoa masuluhisho halisi  kwa matatizo  yanayoikabili jamii  na yana umuhimu katika  kuboresha moja kwa moja maisha na hususani maisha ya watoto,” alisema Okash, akibainisha kuwa kampuni hiyo ya simu  tayari imeshawasaidia  wajasirimali kijamii tisa kupitia mkakati wa waleta mabadiliko wa Tigo (Tigo Digital Changemakers).

 Huu ni mwaka wa sita  ambapo Tigo na Reach-for-Change wanaendesha shindano la kutafuta  wajasiriamali kijamii.
  Mshindi wa mwaka huu  atatangazwa Machi 9.
Mwisho

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa