Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » WACHIMBAJI WADOGO WAMUOMBA RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI KUACHIA MCHANGA ULIOKAMATWA BANDARINI

WACHIMBAJI WADOGO WAMUOMBA RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI KUACHIA MCHANGA ULIOKAMATWA BANDARINI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Wachimbaji wadogo wa madini wamemuomba Rais Dk. John Pombe Magufuli kuwaachia mchanga wa madini uliozuiwa bandarini kutokana na kuwepo kwa mchanga katika bandari kavu huku wakiendelea kutozwa ushuru wa kuhifadhi.

Wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wamesema kuwa mchanga uliozuiwa na bandarini sio wa dhahabu ambao mashine za kuchanjulia ziko hapa nchini.

Mmoja wa wachimbaji hao , King Selemani amesema kuwa mchanga wanaosafirisha kwenda nje ni shaba, Nickel ,Manganise ore ,Zinc ore, Galena pamoja na lead ore ambapo hapa nchini hakuna mtambo wa kuchenjua mchanga huo.

Selemani amesema kuzuiwa kwa mchanga huo kumewaathiri pamoja na kusitisha ajira kwa baadhi ya wafanyakazi katika machimbo ya madini hayo.

Aidha amesema kuwa Rais Dk. John Pombe Magufuli amekuwa mstari mbele hivyo wamemuomba kuwachia kuendelea na biashara hiyo.
Mchimbaji Mdogo wa Madini, King Selemani akizungumza leo na waandishi wa habari juu ya kumuomba Rais Dk.John Pombe Magufuli kutoa ruhusa ya kuwaachia mchanga wa madini uliozuiwa katika bandari ya Dar es Salaam.
Mchimbaji Mdogo na msafirishaji wa Madini , Paul Kalyembe akizungumza na waandishi wa habari juu ya kuwaruhusu kufanya biashara hiyo huku serikali ikisubiri kufanya taratibu zungine za kuwa na kiwanda cha kufanya kazi ya kuchenjua madini katika mchanga wa Nickel, Shaba na madini megine leo jijni Dar es Salaam.picha na Emmanuel Massaka,Glob ya jamii.
Sehemu ya waandishi habari wakiwasikiliza wachimbaji wadogo wa madini leo jijini Dar es Salaam . 
Michuzi Media Group.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa