Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Wachimbaji
wadogo wa madini wamemuomba Rais Dk. John Pombe Magufuli kuwaachia
mchanga wa madini uliozuiwa bandarini kutokana na kuwepo kwa mchanga
katika bandari kavu huku wakiendelea kutozwa ushuru wa kuhifadhi.
Wakizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wamesema kuwa mchanga
uliozuiwa na bandarini sio wa dhahabu ambao mashine za kuchanjulia ziko
hapa nchini.
Mmoja
wa wachimbaji hao , King Selemani amesema kuwa mchanga wanaosafirisha
kwenda nje ni shaba, Nickel ,Manganise ore ,Zinc ore, Galena pamoja na
lead ore ambapo hapa nchini hakuna mtambo wa kuchenjua mchanga huo.
Selemani
amesema kuzuiwa kwa mchanga huo kumewaathiri pamoja na kusitisha ajira
kwa baadhi ya wafanyakazi katika machimbo ya madini hayo.
Aidha amesema kuwa Rais Dk. John Pombe Magufuli amekuwa mstari mbele hivyo wamemuomba kuwachia kuendelea na biashara hiyo.
Mchimbaji
Mdogo wa Madini, King Selemani akizungumza leo na waandishi wa habari
juu ya kumuomba Rais Dk.John Pombe Magufuli kutoa ruhusa ya kuwaachia
mchanga wa madini uliozuiwa katika bandari ya Dar es Salaam.
Mchimbaji
Mdogo na msafirishaji wa Madini , Paul Kalyembe akizungumza na
waandishi wa habari juu ya kuwaruhusu kufanya biashara hiyo huku
serikali ikisubiri kufanya taratibu zungine za kuwa na kiwanda cha
kufanya kazi ya kuchenjua madini katika mchanga wa Nickel, Shaba na
madini megine leo jijni Dar es Salaam.picha na Emmanuel Massaka,Glob ya
jamii.
Sehemu ya waandishi habari wakiwasikiliza wachimbaji wadogo wa madini leo jijini Dar es Salaam .
Michuzi Media Group.
Michuzi Media Group.
0 comments:
Post a Comment