Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » HOSPITALI YA SANITAS YAWEKA KAMBI KWA AJILI YA KUCHANGIA DAMU

HOSPITALI YA SANITAS YAWEKA KAMBI KWA AJILI YA KUCHANGIA DAMU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

image5.JPG

image1.JPG

image4.JPG

image2.JPG

image3.JPG

Kuelekea siku ya kuchangia damu duniani, Hospitali ya Sanitas iliyopo Mikocheni, iliandaa Kambi ya kuchangia Damu Leo Jumanne, Tarehe 13 Juni 2017. 

Katika Kambi hiyo zaidi ya chupa 50 za damu zilikusanywa na Damu Salama. 

Waliochangia Damu ni watu kutoka nje Pamoja na Staff wa Sanitas Hospital. 

Kwa kuchangia chupa moja ya damu, unaweza kusaidia Watanzania watatu. 

Damu inahitajika mahospitalini kwa kuokoa maisha ya Kundi yafuatayo:
- wajawazito waliokuwa na tatizo wakati wa kujifungua
- watoto waliokuwa na upungufu wa damu
- watu waliokuwa na ugonjwa wa sikla
- watu waliokuwa wamepata ajali na wanaofanyiwa upasuaji

"Kuna Uhaba wa Damu, Hakikisha unaonyesha uzaleno na upendo wako kwa Watanzania wenzio kwa kuchangia damu na kuokoa maisha yao" - Alisema Dr. Sajjad Fazel, meneja msaidizi wa Hospitali ya Sanitas

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa