Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » WASHIRIKI WA SHINDANO LA BONGO STYLE WAENDESHEWA SEMINA KUHUSU PICHA,MITINDO NA UANDISHI WA FILAMU

WASHIRIKI WA SHINDANO LA BONGO STYLE WAENDESHEWA SEMINA KUHUSU PICHA,MITINDO NA UANDISHI WA FILAMU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Bi. Joyce Msigwa ambaye ni Mratibu wa Faru Arts and Sports Development Organization (FASDO) akitoa maelezo kwa washiriki wa  'Bongo Style Competition'  2017, kuhusiana na asasi ya FASDO
Mwezeshaji Bw. Erick Chrispin akitoa semina kwa washiriki wa Bongo Style namna ya kujiongoza wenyewe katika maswala ya Fedha,Muda na uongozi.
Baadhi ya washiriki wa shindano la Bongo Style 2017, wakiwemo wapiga picha,waandishi wa miswada ya Filamu na wabunifu wa mitindo upande wa mavazi wakiwa wanafanya zoezi waliopewa na mwezeshaji Bw. Erick Chrispin (ambaye hayupo pichani)
Baadhi ya Washiriki wa Bongo Style Competition 2017 wakiwa wanafanya kazi waliyopewa na mwezeshaji Bw. Erick Chrispin (hayupo pichani) baada ya kumaliza semina yake.
 Mkufunzi na Mtaalam wa maswala ya Picha Bw. Iddy John akitoa somo juu ya maswala ya picha kwa washiriki wa Shindano la Bongo Style kundi la  Picha
Mbunifu maarufu wa Mitindo ya mavazi Martin Kadinda akitoa somo kwa washiriki  kundi la mitindo
Washiriki wa kundi la  Ubunifu wa mitindo upande wa  mavazi wakipewa vitendea kazi.
Bi. Christina Pande(aliyesimama) ambaye ni Mtunzi na muongozaji wa Filamu, akiwapa darasa vijana ambao wapo katika kundi la Uandishi wa  miswada ya Filamu shindano la Bongo Style 2017.
Picha zote na Fredy Njeje.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa