Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Benki ya UBA yawavutia wateja katika maonyesho ya Sabasaba

Benki ya UBA yawavutia wateja katika maonyesho ya Sabasaba

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Afisa wa Bank ya UBA Tanzania, Bi Mtinta Joseph Ringa pamoja na afisa wa bank Bw. Sihika Malunguja wakifurahi kumuhudumia mmoja wa wateja aliyetembelea banda la bank ya UBA Tanzania katika Maonyesho ya 41 ya kibiashara Tanzania yaliyoanza hivi karibu. Bank ya UBA inawakaribisha wateja wote kuweza kufika katika banda lao kwaajili ya kujipatia huduma mbalimbali za kibenki ikiwemo na kufungua akaunti na kujipatia kadi mpya ya Mastercard ambayo unaweza kuwa nayo bila kuwa na akaunti.
 Afisa wa benki ya UBA Tanzania, Bw Fahimu Zuberi akimpatia maelezo kuhusiana na kadi mpya za mastercard mmoja wa wateja waliotembelea banda la benki hiyo lililopo katika banda la Sabasaba kwenye maonyesho ya 41 ya kibiashara ya kimataifa yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Jijini Dar Es Salaam
 Afisa wa benki ya UBA Tanzania, Bw Fahimu Zuberi akiendelea kumpatia maelekezo ya kina kuhusiana na kadi mpya mpya za mastercard ambazo mteja anaweza kuwa nayo bila kuwa na akaunti ya benki
Wafanyakazi wa benki ya UBA Tanzania waliopo kwenye banda lao katika maonyesho ya 41 ya kimataifa ya biashara wakiwa katika picha ya pamoja huku wakifurahia kuwahudumia baadhi ya wateja waliofika katika banda lao huku wakiwakaribisha wateja kufika katika banda lao na kujipatia huduma mbalimbali za kibenki. Picha zote na Josephat Lukaza - Lukaza Blog

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa