Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akizungumza na
wafanyabiashara wa Stendi ya Mabasi Ubungo,wajumbe wa Kamati ya Fedha na
uchumi ya Halmashauri ya Jiji alipofanya ziara ya kushtukiza katika
kituo cha mabasi ubungo jana,kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Jiji.
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akiwasikiliza Askari
Polisi wa Ubungo alipofanya ziara ya kushtukiza jana katika kituo cha
mabasi yaendoyo mikoani. katikati Mwenye Shati jeupe ni Diwani wa kata
ya segerea ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya fedha na uchumi ya
Halmashauri ya Jiji, Patrick Asenga.wa kwanza kushoto ni Meneja wa Kituo
cha mabasi ubungo Iman Kasagara.
Meneja wa Kituo cha mabasi Ubungo , Iman Kasagara
akizungumza na waandishi wa habari leo mara baada ya Mstahiki Meya wa
Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita na Kamati ya fedha na Uchumi
walipofanya ziara ya kushtukiza katika kituo cha mabasi Ubungo.
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita
akizungumza na waandishi wa habari jana alipofanya ziara ya kushtukiza ya
kutembelea kituo cha mabasi ubungo.
Mbunge wa Jimbo la Ubungo, ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Madiwani la
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam akizungumza na waandishi wa habari
jana kwenye ziara iliyofanywa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam
na Kamati ya fedha ya jiji.
0 comments:
Post a Comment