Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » WAFANYABIASHARA CHINA WAPIGWA MSASA

WAFANYABIASHARA CHINA WAPIGWA MSASA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Imeandikwa na Shadrack Sagati
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema.
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeanza mkakati wa kuwapiga msasa wafanyabiashara kutoka China ili watambue kodi wanazotakiwa kulipa serikalini na taratibu wanazotakiwa kufuata wakati wanapokuwa wanaishi nchini.
Kwa kuanzia jana, TRA ilianza kuwaelimisha wafanyabiashara wa China, wanaofanya kazi katika wilaya ya Ilala, ambao mamlaka hiyo ilikiri kuwa wamekuwa hawafuati taratibu kadhaa za kulipa kodi.
Mkutano huo umeandaliwa kwa ushirikiano na wilaya ya Ilala na idara ya uhamiaji. Meneja wa Elimu kwa Walipa Kodi wa TRA, Diana Masalla alisema jana kuwa maeneo ambayo wanawaelimisha wafanyabiashara hao wa China ni ulipaji wa kodi ya mapato, ulipaji wa kodi ya ufundi stadi, ulipaji wa kodi wanayokatwa wafanyakazi (PAYEE) na matumizi ya mashine za malipo za kielektroniki (EFDs).
Masalla alisema pia kwenye semina hiyo, watawaelimisha wafanyabiashara namna ya kuandaa hesabu za biashara, kiasi cha kodi kinacholipiwa kodi kwenye biashara na taratibu zingine za kodi.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam, Sophia Mjema alisema baada ya kuwasajili wamachinga katika wilaya yake ili wachangie kodi serikalini, sasa wameanzisha mkakati kuhakikisha kuwa wafanyabiashara kutoka China wanalipa kodi stahiki serikalini.
Alisema katika semina hiyo, watawaelimisha taratibu za kupata vibali vya kuishi nchini na kufanya kazi nchini, namna ya kulipa kodi kwa biashara wanayofanya na wafuate taratibu zingine za nchi ili wasiingie kwenye matatizo.
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa