Na: Lilian Lundo -
MAELEZO
Serikali kupitia
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeanzisha rejesta
ya wanaohisiwa kuwa na ugonjwa wa kifua kikuu itakayowekwa katika kila ngazi ya utoaji wa huduma za Afya
hapa nchini.
Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameyasema hayo, leo
Mjini Dodoma, katika mkutano wa kupitia utekelezaji wa mkakati wa uboreshaji wa
kasi ya uibuaji wa wagonjwa wa kifua kikuu nchini.
Ummy amesema Serikali inayo wajibu wa
kuhakikisha mkakati huo unatekelezwa kwa ufanisi uliokusudiwa, ili kufikia
lengo hilo.
Kutokana nna dhamira hiyo njema Wizara kwa mara ya kwanza
imeanzisha rejesta mpya ya wanaohisiwa kuwa na kifua kikuu itakayowekwa katika
kila ngazi ya utoaji wa huduma za Afya hapa nchini.
“Tayari rejesta hizi zimesambazwa na kuanza kutumika katika mikoa
16 iliyoanza kutekeleza zoezi hili,” amesema Ummy.
Waziri Ummy aliongeza kuwa mkakati wa uboreshaji kasi ya uibuaji
wagonjwa wa kifua kikuu ni mkakati uliojaa mbinu za kiuendeshaji ili kuvipa
uwezo vituo vya huduma za Afya kufanya uchunguzi wa kina kwa kila mteja
anayepata huduma vituoni na kuwapata wote wenye kuugua kifua kikuu na
kuwaanzishia matibabu.
Ummy amesema mkakati huo unahusisha zana zinazotoa mwanga na
kuangaza njia bora za kuchunguza kifua kikuu na kubaini wote wenye kuugua
katika jamii mijini na vijijini.
Vile vile amesema, mkakati huo umejaa mbinu za kiuendeshaji ili
kuvipa uwezo vituo vya huduma ya Afya kufanya uchunguzi wa kina kwa kila mteja
anayepata huduma vituoni na kuwapata wote wenye kuugua kifua kikuu pamoja na
kuwaanzishia matibabu.
Pia utatoa fursa kwa kila kitengo kujitathmini ili kuweka misingi
timilifu ya uchunguzi wa kifua kikuu kwa wateja wote wanaohudhuria matibabu
katika eneo husika.
Aidha, amesema kuwa utekelezaji wa mkakati huo ulianza mnamo
Julai, 2016, ambapo ni mwaka mmoja sasa tokea vituo vya mwanzo katika Mikoa ya
Mbeya na Dodoma ianze kuweka msukumo mpya. Kuanzia hapo, Mikoa 16, wilaya 48 na
vituo 187 nchini kote vimeweza kuanza utekelezaji.
Masuala ya ubora wa huduma za afya yamepewa kipaumbele katika
mkakati mpya uliotolewa na Shirika la Afya Duniani wa kutokomeza kifua kikuu
ifikapo mwaka 2035.
0 comments:
Post a Comment