Na: Immaculate Makilika- MAELEZO
Shirika la Uzalishaji
Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT),
linatarajia kuanzisha kiwanda cha kusindika minofu ya nyama ya ng’ombe
na samaki na kampuni ya kusambaza nyama
kwa nia ya kuunga mkono azma ya Serikali ya awamu ya tano ya kuelekea katika
uchumi wa viwanda.
Akizungumza katika
kipindi cha TUNATEKELEZA kinachoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Idara ya Habari, (MAELEZO) na kurushwa na
kituo cha televisheni cha TBC1,
Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT
Brigedia Jenerali Charo Yateri
alisema kuwa shirika hilo pia
limedhamiria kutoa mafunzo kwa
vijana kupitia miradi mbalimbali ambayo ipo chini ya shirika hilo.
“SUMA JKT imeendelea kujiimarisha kupitia
miradi yake ya kilimo, huduma za
ulinzi, uvuvi pamoja na ufugaji, ambapo ina viwanda vya kusindika na kuchakata
mazao, na asali ambapo kupitia miradi na viwanda hivyo imetoa ajira 4,500 kwa vijana nchini” alisema
Brigedia Jenerali Yateri.
Alitaja viwanda hivyo
kuwa ni viwanda vya kusindika asali mkoani Tabora, viwanda vya kusindika na
kuchakata nafaka vilivyopo Mlale mkoani Ruvuma
na Mafinga mkoani Njombe.
Mbali na hayo,
Brigedia Jenerali Yateri alisema kuwa SUMA JKT ina miradi mbalimbali ikiwemo ya
kujenga majengo ya Halmashauri, barabara
kwa gharama nafuu, ubora na uharaka Nna wana mpango
wa kujenga nyumba za wanajeshi kwa ajili
ya kuwakopesha.
“ Tunaendelea kufanya
mazungumzo na benk ya Azania ili tujenge
nyumba za wanajeshi ambapo wataweza kupewa mikopo ya kununua nyumba hizo, na
baadae tutaanza kujenga nyumba kwa wananchi” alisema Brigedia Jenerali Yateri.
Alitaja huduma nyingine zinazofanywa na shirika hilo
kuwa ni pamoja na kuuza zana bora za
kilimo kama matrekta, pampu za maji kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji,
kufundisha jamii kilimo, uzalishaji wa mbegu bora za nafaka na mradi wa mabwawa ya kufuga samaki katika vizimba
vya ziwa Victoria
Aidha, Brigedia
Jenerali Yateri alisema SUMA JKT inajivunia
miradi hiyo sambamba na kuwa na
kilimo cha mazao ya biashara kama vile
kahawa mkoani Mbeya na mchikichi mkoani
Kigoma, sambasamba na uwezo wa
kujitegemea kwa asilimia 55, huku ikipata ruzuku ya serikali asilimia 45
tu.
Shirika la Uzalishaji
Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT), lilianzishwa mwaka 1982, kwa tamko
la Rais chini ya sheria ya uanzishaji wa mashirika ya ummakwa lengo la
kuisaidia serikali kupunguza gharama za
kuendesha mafunzo kwa vijana wanaopatiwa ujuzi wa aina mbalimbali ili kutumikia
Jeshi la Kujenga Taifa pamoja na Taifa
kwa ujumla.
0 comments:
Post a Comment