Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » TTCL YAINGIA RASMI KWENYE MFUMO WA KUTUMA PESA KWA NJIA YA SIMU

TTCL YAINGIA RASMI KWENYE MFUMO WA KUTUMA PESA KWA NJIA YA SIMU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na: Paschal Dotto Na Thobias Robert -MAELEZO
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amezindua rasmi mfumo wa huduma ya kutuma pesa kwa njia ya simu za mkononi wa kampuni ya mawasiliano ya TTCL ujulikanao kama “TTCL PESA” katika Makao Makuu ya Kampuni hiyo Jijini Dar es Salaam.
Akizindua mfumo huo Jijini Dar es Salaam leo, Makamu wa Rais amesema kuwa, TTCL imetekeleza agizo la serikali ya awamu ya tano lililoyataka mashirika yote ya Umma yajiendeshe yenyewe kwa faida, pia kuwahudumia wananchi na kuondoa urasimu ambao umekuwa ukifanywa na Makampuni ya kigeni.
“Kuzinduliwa kwa huduma hii ni udhibitisho mwingine kwamba TTCL kama kampuni inayomilikiwa na serikali imejidhatiti kutekeleza kwa vitendo azma ya Dkt Johm Pombe Magufuli inayotaka Mashirika yote ya Umma kujiendesha kwa faida na kutoa gawio kwa serikali’’ . Alisema Makamu wa rais.
Kampuni ya TTCL inaimarika kiutendaji ili kuendana na mabadiliko ya kidijitali, kwa kudhihirisha hilo waliweza kuibuka washindi wa kwanza katika maonesho ya 41 ya Kimataifa ya kibiashara ya Sabasaba katika utoaji wa huduma ya mawasiliano nchini Tanzania.
Kuanzishwaa kwa huduma kutafungua fursa za kibiashara na utoaji wa huduma kwa watu mbalimbali yakiwemo maeneo ya vijijini, kama kutuma na kupokea pesa, kulipia huduma mbalimbali kama vile bili za umeme na Maji, pia koungeza pato la taifa kupitia kodi ya miamala itakayokuwa inafanywa.
Mafanikio ya Kampuni hiyo yamechagizwa na uamuzi wa serikali wa kuirudisha mikononi mwake na kuiundia bodi mpya na menejimenti ambayo jukumu lake kubwa ni kuiendesha kiushindani na kibiashara ili kuendana na mabadiliko ya soko.
Awali akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa bodi ya TTCL Bw. Omary Nundu amesema kuwa, Kampuni hiyo ina mpango wa kuanzisha utengenezaji wa simu hapa nchini, lakini pia ametoa wito kwa wananchi kuanza kutumia huduma ya TTCL kwani ni kampuni ya serikali hivyo watadhihirisha uzalendo kwa nchi yao pamoja na kuikuza Kampuni hiyo kimapato.
Akizungumza kwa niaba ya Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Naibu Katibu Mkuu Dkt. Maria Sasabo amesema kuwa serikali inazidi kuimarisha Kampuni hiyo ili iweze kuingia katika soko la ushindani wa mawasiliamno na makapmuni menginhe yanayotoa huduma hizo, kama vile, Vodacom, Airtel, Tigo, Halotel, Smart pamoja na Zantel.
TTCL ni kampuni pekee nchini yenye mtandao mkubwa wa mawasiliano unaotumika katika ofisi za serikali na baadhi ya Taasisi binafsi, kwa kuzingatia kuwa wao ndio wamiliki wa mkongo wa taifa wa mawasiliano ambao umeleta mabadiliko makubwa katika Nyanja ya mawasiliano hapa nchini.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa