NA; EVELYN MKOKOI
NAIBU
Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina
,amesitisha uchimbaji na uchotaji wa mchanga kiholela katika maeneo
yasiyo rasmi.
Pia ametoa siku 30 kwa Halmashauri za
Manispaa za Jiji la Dar es Salaam kubaini na kutenga maeneo ya uchimbaji
ya mchanga ambayo yapo ndani ya manispaa zao yatakayo ruhusiwa kwa
zoezi hilo kisheria.
Akitoa agizo hilo Dar es Salaan leo,wakati
wa ziara ya kutembelea Mto Nyakasangwe uliopo maeneo ya Boko Kata ya
Bunju alisema kama kuna maeneo ambayo wananchi wanaweza kufika Kwa
urahisi, manispaa zinapaswa kuyatembelea maeneo hayo na kuyabaini kama
kunauwezekano wakuchimba mchanga.
Alisema ndani ya mwezi mmoja
manispaa hizo zinatakiwa kuandaa utaratibu mfupi wa kutenga maeneo hayo
ikiwemo utoaji wa vibali kutoka Wizara ya Nishati na Madini,Halmashauri
pamoja na Nemc.
“Halmashauri zote zilizo na eneo ambalo linaweza
kuruhusiwa kuchota mchanga hakikisheni mnatembelea maeneo hayo na
kufata taratibu zote za utoaji wa vibali ambapo maeneo mengine yawe ya
uchotaji wa mchanga,”alisisitiza Mpina
Alisema watafanya
Operasheni ya usiku na mchana kuhakikisha watu watakaoendelea kuchimba
mchanga na kuchota mchanga sehemu ambazo haziruhusiwi watachukuliwa
hatua ikiwa ni pamoja na kutozwa faini zilizopo kisheria na kufikishwa
mahakamani.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Bunju Bw. Kateni
Nassor Msangi alimshukuru Mpina kwa kufanya ziara katika eneo hilo na
kuiomba serikali kufanya utaratibu wa kujengea mawe katika kuta za kingo
yam to huo ambao umeharibika vibaya, ili kuweza kunusuru mazingira ya
mto huo kuharibika pamoja na kunusuru makazi yao.
0 comments:
Post a Comment