Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » USHIRIKA WA WACHINJA KUKU KISUTU WENYE MALENGO MAKUBWA YA UWEKEZAJI

USHIRIKA WA WACHINJA KUKU KISUTU WENYE MALENGO MAKUBWA YA UWEKEZAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Kuku wakiendelea kuandaliwa ndani ya Soko la Kisutu. Picha zote na MaendeleoVijijini.
Mazingira ya ndani yanaridhisha kutokana na usafi ambao unazingatiwa sana na wahusika licha ya changamoto za hapa na pale.
Hawa ni wanaushirika wa Kisutu Poultry Farm Cooperative Society (KIPOCOSO), ambao wamekuwepo katika soko hilo kwa zaidi ya miaka 28 na ndio waanzilishi wa kuchinja kuku jijini Dar es Salaam.
Na Daniel Mbega, MaendeleoVijijini.

SAUTI za kuku zinasikika hata ukiwa nje ya jengo dogo ndani ya Soko la Kisutu jijini Dar es Salaam, lakini ghafla zinakoma na zinasikika nyingine.
Siyo kwamba kuku hao wanahitaji chakula ama wanacheza, bali hapa ni machinjio, na sauti zinapokoma ujue tayari zimekwishapigwa kisu na zinaandaliwa kwa ajili ya kitoweo.

Nje ya jengo hilo unaweza kuwa umekuta akinamama wengi wakiwa wamelundikana huku wakiwa wamekalia ndoo zao.Hawa nao wanasubiri huduma, wanataka kununua utumbo, miguu pamoja na vipapatio vya kuku hao wanaochinjwa ili wakafanye biashara.

Akinamama hawa wanatoka katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam na hapa Kisutu ndiko mahali pekee ambako wanaweza kupata bidhaa hiyo wanayokwenda kuuza mitaani.Bila shaka baadhi yetu tumekutana ama tumewakuta akinamama wakiuza firigisi na utumbo mitaani, basi amini kwamba asilimia kubwa wanapata bidhaa hiyo katika eneo hili la Kisutu.

Ukiingia ndani ya jengo hilo usishangae ukasalimia usiitikiwe na watu wengi, japokuwa waliomo ni wengi.Kabla hujajua usimame wapi, utasikia sauti ya mtu akikutaka radhi kwamba anaomba kupita ama anataka kuweka mzigo.Naam. Kila mtu hapa yuko ‘busy’ na kazi inakwenda mtindo mmoja, na hata kutokukuitikia si kwamba wanafanya kiburi ama hawajakuona, la hasha. Kwa sababu wanataka kuhakikisha kazi wanayoifanya inakuwa katika hali bora hasa ikizingatiwa kwamba hicho ni chakula kwa afya ya binadamu.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa