Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » WATENDAJI TOENI USHIRIKIANO WA KUWEZESHA KUKAMILIKA KWA MRADI WA UENDELEZAJI WA JIJI LA DAR ES SALAAM (DMDP) – WAZIRI JAFFO

WATENDAJI TOENI USHIRIKIANO WA KUWEZESHA KUKAMILIKA KWA MRADI WA UENDELEZAJI WA JIJI LA DAR ES SALAAM (DMDP) – WAZIRI JAFFO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo akizungumza na katika uzinduzi wa jengo la ofisi na Maabara za mradi  wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP), leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo akikabidhiwa  mfano ufunguo wa jengo la mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP)  kutoka kwa Mratibu wa Miradi, Devis Shemangali unaofadhiliwa  na Banki ya Dunia  leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo la mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP) leo jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo amewataka watendaji wa Manispaa ya Temeke kutoa ushirikiano ili kuwezesha kukamilika kwa mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP) na watendaji watakaoshindwa kutoa ushirikiano huo watashughulikiwa.
Akizungumza leo wakati uzinduzi wa jengo la ofisi na Maabara za mradi  wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP) lililojengwa katika Manispaa ya Temeke, Jaffo amesema mradi huo utawezesha manispaa ya Temeke kuwa ya sura mpya na kuwa mfano kwa jiji la Dar es Salaam.
Amesema mradi utawezesha kujengwa kwa barabara na mifereji na hivyo kupunguza msongamano wa magari.
Amesema mradi huo ambao unafadhiliwa na Benki ya Dunia (WB) utatekelezwa katika jiji zima la Dar es Salaam katika kupanga mji kuwa na makazi bora yenye huduma zinazoendana na makazi hayo.
“Temeke mmekuwa na  bahati ya kuwa ya kwanza kutekeleza mradi huu, shirikianeni kuifanya Temeke kuwa ya kisasa kwa kuondoa Temeke  iliyokuwepo zamani isiyokuwa na miundombinu rafiki kwa makazi ya wananchi,” amesema.
Mratibu wa mradi huo katika manispaa ya Temeke, Edward Simon amesema Shilingi bilioni 265 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi barabara na mifereji. Amesema jumla ya kilometa 91 za barabara za ndani zitajengwa kwenye manispaa hiyo.
Amesema mradi huo ukikamilika utawezesha barabara kupitika na kupunguza mafuriko kutokana na kutengenezwa mifereji.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa