Home » » WAZIRI MWAKYEMBE AFANYA ZIARA BASATA KUANGALIA MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA MAONYESHO

WAZIRI MWAKYEMBE AFANYA ZIARA BASATA KUANGALIA MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA MAONYESHO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Mtendaji Mkuu Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza (kushoto) akimuonyesha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (mwenye kofia ya blue) eneo la jukwaa lilivyozingatia ubora wa maonyesho alipofanya ziara katika taasisi hiyo kujua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa maonyesho wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam.
Mkandarasi wa ujenzi wa ukumbi wa BASATA Bw. Novart Ludovick (wapili kushoto) akimweleza Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (mwenye kofia ya blue) maendeleo ya ujenzi ulipofikia alipofanya ziara katika taasisi hiyo kujua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa maonyesho wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza (katikati) akimuonyesha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) picha inayoonyesha muonekano wa ukumbi wa BASATA utakavyokua baada ya kumalizika alipofanya ziara katika taasisi hiyo kujua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa maonyesho wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akizungumza na watumishi wa BASATA (hawapo pichani) baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mtendaji Mkuu BASATA Bw. Godfrey Mngereza.
Mtendaji Mkuu BASATA Bw. Godfrey Mngereza (kushoto) akimkabidhi zawadi ya picha ya tingatinga Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa BASATA pamoja na kuzungumza na watumishi wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Maendeleo ya Sanaa Bibi. Leah Kihimbi.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kushoto) akisikiliza wimbo uliotungwa na kuimbwa na mwanamuziki kutoka Kongo unaosifia Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa BASATA pamoja na kuzungumza na watumishi wa BASATA jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mtendaji Mkuu BASATA Bw. Godfrey Mngereza. Picha na Genofeva Matemu -WHUSM

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa