Home » » HECHE: MADHILA YA UCHAGUZI YALIVYOFIKISHA CHADEMA ‘NO REFORMS, NO ELECTION’

HECHE: MADHILA YA UCHAGUZI YALIVYOFIKISHA CHADEMA ‘NO REFORMS, NO ELECTION’



Na Karama Kenyunko Michuzi Tv


SHAHIDI wa tano wa utetezi katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, John Heche, ameieleza Mahakama namna matukio mbalimbali aliyodai kuyashuhudia katika chaguzi yalivyosababisha chama hicho kufikia msimamo wa “No Reforms, No Election” (Bila Mabadiliko, Hakuna Uchaguzi).

Heche, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, ametoa ushahidi huo leo Septemba 9, 2026, katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, mbele ya Jopo la Majaji watatu wakiongozwa na Jaji Dustun Ndunguru.

Akijibu maswali ya Lissu, Heche amesema Desemba 2, 2024, Kamati Kuu ya CHADEMA ilikaa na kujadili masuala mbalimbali yaliyohusu chaguzi, ikiwemo ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi, kuenguliwa kwa wagombea wa chama hicho na matukio ya mauaji yaliyohusishwa na chaguzi.

Heche amesema kutokana na hali hiyo, hususani uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 na chaguzi nyingine alizoshiriki na kuzishuhudia, chama hicho kiliona kuwa hazikuwa chaguzi za kawaida bali “uchafuzi”, jambo lililopelekea Kamati Kuu chini ya Mwenyekiti wa wakati huo, Freeman Mbowe, kufikia msimamo wa “No Reforms, No Election.”

Amesema mabadiliko yaliyokuwa yakihitajika yalihusisha marekebisho makubwa ya Katiba na sheria, pamoja na kuondoa madaraka makubwa ya Rais katika uundaji wa Tume ya Uchaguzi na uteuzi wa watendaji wa uchaguzi.


SOURCE : MICHUZI BLOG


0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa